MKAZI WA NAMANYERE AMWAGIWA TINDIKALI

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,Kaster Ngonyani akitoa taarifa kwa wanahabari leo katika ofisi za jeshi hilo mkoa.

Na Walter Mguluchuma,Katavi

Mtu mmoja  aliyejulikana kwa jina la   Ernest  Lyoba (61) Mkazi wa  Kijiji cha  Namanyere Kata ya Majimoto Wilaya ya Mlele  amejeruhiwa vibaya   katika sehemu yake ya uso na  mgongoni baada ya kumwagiwa  tindikali  na watu wasio julikana wakati akiwa njiani  anaelekea nyumbani kwake.

Mtu mmoja  aliyejulikana kwa jina la   Ernest  Lyoba (61) Mkazi wa  Kijiji cha  Namanyere Kata ya Majimoto Wilaya ya Mlele  amejeruhiwa vibaya   katika sehemu yake ya uso na  mgongoni baada ya kumwagiwa  tindikali  na watu wasio julikana wakati akiwa njiani  anaelekea nyumbani kwake.

Kamanda wa  Polisi wa Mkoa wa Katavi  Kaster Ngonyani amewaambia wandishi wa  habari kuwa tukio hilo la  kikatili  la kusitishia  limetokea  June  25 huko  katika eneo la  Kijiji cha  Namanyere.

Amebainisha kuwa siku ya tukio   mhanga  alikuwa  yuko  njiani  akiwa  anaelekea   nyumbani kwake  majira  ya saa tisa   alisiri  mara  baada ya kuwa amemaliza shughuli zake za kujitafutia  riziki ndipo watu wasio julikana walimmwagia tindikali  sehemu za  usoni na mgongoni na kumjeruhi vibaya na kisha watu hao walitokomea mahali  pasipo julikana .

Kamanda   Ngonyani amesema baada ya  mhanga kuwa  amemwagiwa tindikali hiyo  alipiga kelele za kuomba  msaada na baada ya muda mfupi watu walifika kwenye eneo hilo na kumkuta   Ernest Lyoba akiwa  amejerihiwa  vibaya .

Ameeleza  wasamalia hao wema walimchukua  mhanga huyo na kumkimbiza kwa haraka hadi  kwenye    Hospitali ya  Halmashauri ya  Mpimbwe kwa ajiri ya matibabu hata hivyo  kutokana na kuwa amejeruhiwa  vibaya  mhanga alipewa rufaa ya  kwenda  kupatiwa  matibabu katika  Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi .

Hata hivyo baada ya kuwa amefikishwa  katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi  alipewa    tena ya kwenda kupatiwa matibabu zaidi   kwenye    Hospitali ya Rufaa ya KMC ya  Mkoani   Kilimanjaro ambako  amelezwa hadi sasa.

Kamanda  Ngonyani  amesema  juhudi za  kuwasa watuhumiwa  hao  zinaendelea kufanywa na jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi ili kuhakikisha linawakamata nakuwa tia  nguvuni na  kuwafikisha mara moja  Mahakamani  ili wakajibu  mashitaka ya tuhuma  zitakazo kuwa  zinawakabili.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages