POLISI KATAVI WAWAHAKIKISHIA WANANCHI USALAMA EID AL ADHA.

 

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,Kaster Ngonyani akizungumza na wanahabari leo katika ofisi za jeshi hilo ambapo amesisitiza kuwa Jesho hilo limejipanga kuimarisha usalama kwenye sikukuu ya EID AL HAJJ

Na Walter Mguluchuma,Katavi .

Jeshi  la Polisi Mkoa wa  Katavi  limewahakikishia wananchi wa Mkoa huu kusherekea   sherehe za EID AL HAJJ k wa  Amani  na  utulivu  kutoka na jeshi  hili  lilivyojipanga na   walivyoimarishaulinzi wakati  wa kipindi cha sikukuu na baada ya sikukuu  katika kuhakikisha Mkoa wa Katavi unaendelea kuwa salama.

Jeshi  la Polisi Mkoa wa  Katavi  limewahakikishia wananchi wa Mkoa huu kusherekea   sherehe za EID AL HAJJ k wa  Amani  na  utulivu  kutoka na jeshi  hili  lilivyojipanga na   walivyoimarishaulinzi wakati  wa kipindi cha sikukuu na baada ya sikukuu  katika kuhakikisha Mkoa wa Katavi unaendelea kuwa salama .

Kaulu hiyo ya jeshi la polisi Mkoa wa Katavi  imetolewa  na   Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani  wakati  alipokuwa akiongea na wandishi wa  Habari ofisini kwake  .

 Amesema  Jeshi la Polisi     Mkoa wa Katavi linawahakikishia wananchi wa Mkoa huu  kuwa wamejipanga  ipasavyo  kuhakikisha  wakati wa kipindi cha sikukuu ya EID  AL  HAJJ na  baada ya sikukuu Amani na utulivu  katika Mkoa wa Katavi inaendelea kuwepo .

Ameeleza kuwa wakati wa  sikukuu  wananchi wawe     na  Amani katika kusherkea sikukuu hiyo  kwa usalama  kwani  polisi  wamejipanga kufanya doria mbalimbali kwenye maeneo yote ya Mkoa huu  na kwenye barabara zinazo toka na kuingia  ndani ya mkoa .

Kwani muda wote watakuwa wanazunguka kwa kufanya doria za  miguu , gari pikipiki  kwenye maeneo yote  hivyo kama  kutakuwa na tukio  lolole na kuta kuwepo  kwa viashiria vya uvunjwaji wa Amani  wananchi watowe taarifa mara moja ili hatua za haraka ziweze  kuchukuliwa .

Aidha  jeshi la  polisi  limeweza kufanikiwa  kuwakamata watuhumiwa wawili wakiwa na  Televisheni   tatu inchi  42  aina ya   Philips ,Hisense  inchi  43 Televisheni  aina ya  Samsang  inchi  43.

Kamanda  Kaster  Ngonyani  ametaja mali  nyingine walizokamatwa nazo watuhumiwa kuwa ni  Radio  sabusa moja  aina ya    seapiano  na  baiskeli  moja  aina ya  ngamia  mali hizo zote zinazosadikiwa kuwa ni za wizi  wamekamatwa nazo wakiwa wamezificha ndani ya nyumba zao wanazo ishi.

Amewataja watuhumiwa hao kuwa ni  Hassan  Ramadhan na   Vicent  Ndika  wote wakazi wa Mtaa wa Kwalakwacha  Nsemlwa  ambapo jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linaendelea kuwashikilia watuhumiwa hao

Kamanda  Ngonyani  anatowa wito kwa  wananchi  walioibiwa mali  za  aina hiyo  kufika  katika kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpanda  wakiwa na risiti  zenye kuonyesha uhalali wa kuzitambua  mali hizo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages