![]() |
| Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi,Kaster Ngonyani akizungumnza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu taarifa mbalimbali za uhalifu. |
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Katavi Kaster Ngonyani amewaambia
wandishi wa Habari watuhumiwa hao wa uhalifu wamekamatwa kufatia msako mkali
unao uendelea kufanywa na jeshi la Polisi
Mkoa wa Katavi katika maeneo mbalimbali ya Mkoa huu wa kuwasaka watu wote
wanao jihusisha na matukio ya uhalifu .
Amesema watuhumiwa hao 34 wamekamatwa katika kipindi cha mwezi
januari 2026 katika watuhumiwa hao 3
wamekamatwa wakiwa na nyaraza Serikali meno sita ya tembo
nyama ya pori Tembo kilo 71, watuhumiwa 9 wamekatwa wakiwa na bunduki aina ya gobore 8 na
risasi zake 63 na shortgun moja na
risasi 12 watuhumiwa hao wamekuwa
wakijihusisha na uwindaji haramu wa
wanyama pori.
Kamanda Ngonyani amesema katika
msako wamefanikiwa pia kuwakamata
watuhumiwa 8 wakiwa na dawa za kulevya aina ya
Bangi kilo 70 na
kete 320 pia watuhumiwa watatu
wamekamatwa wakiwa na noti bandia 10 za dola 100 na noti 323 za tshs
zote zikiwa na namba moja DF 5893401.
Kwa upande wa makosa ya usalama
barabarani kwa kipindi
hicho cha mwezi wamefanikiwa kukamata makosa 2,351 ya ukiukwaji wa sheria
za usalama barabarani ikiwa ni
katika jitihada zinazo endelee kufanywa na jeshi hilo za
kuzuia ajari za barabarani .
Kamanda Ngonyani ametowa wito kwa
wananchi wa Mkoa wa Katavi kuacha tabia
ya kujihusisha na vitendo vya
uhalifu kwani kufanya hivyo watambue kuwa wataishia
mikononi mwa jeshi la polisi ambao muda wote wapo kazini.

