CRDB BENKI KUWA INUA WANAWAKE NA VIJANA KIUCHUMI


Meneja wa Benki ya CRDB benki akizungumnza na wanawake na Vijana wajasiliamali wakati wa kutambulisha fursa ya utoaji wa Mikopo kwa wanawake na vijana inayo julikana kama IMBEJU.

Na Paul Mathias,Katavi

Wanawake na vijana Wajasiliamali katika Mkoa wa Katavi wameobwa kuwa waaminifu katika kurejesha fedha wanazopatiwa na Benki ya CRDB ili kuendelea kukuza Biashara yao kuptia mikopo hiyo nafuu inayotolewa na Benki hiyo.

Msitahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry akifungua hafla ya utambulisho wa huduma ya utoaji Mikopo kwa wanawake na Vijana Chini ya Benki ya CRDB benki

Wanawake na vijana Wajasiliamali katika Mkoa wa Katavi wameobwa kuwa waaminifu katika kurejesha fedha wanazopatiwa na Benki ya CRDB ili kuendelea kukuza Biashara yao kuptia mikopo hiyo nafuu inayotolewa na Benki hiyo.

Wito huo umetolewa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry wakati wa Hafla ya kutambulisha Fursa ya utoaji wa Mikopo kwa Vijana na wanawake inayotolewa na Benki ya CRDB  inayojulikana kama IMBEJU.

‘’niendelee kusisitiza uaminifu uadilifu ndio kitupekee ambacho kinaweza kutuondelea changamoto hizi za ukosefu wa Mitaji tukiwaa waaminifu Benki itaendelea kutushika Mkono wakikuona wewe unafanya vizuri kwenye Mokopo huu wataweza kukuweka kwenye mikopo mikubwa ‘’amesema sumry

Amesema fursa hiyo ya utoaji wa mikopo kwa wanawake na vijana wajasiliamali isiyo kuwa na Dhamana wala Riba Masahrti Magumu itapunguza malalamiko kwa wanawake ambao wamekuwa wakipata changamoto ya liba Kubwa kwenye taasisi za fedha za mitaani maalufu kama mikopo umiza.

‘’nimekuwa nikipokea malalamiko mengi kwa akina mama wajasiliamali hasa wa Mpanda wamekuwa wakilalamikia sana hizi taasisi zinazo toa mikopo chechefu fursa hii ya IMBEJU kupitia CRDB Benki inakuja kutatua changamoto hizo za utoaji wa mikopo chechefu kwa wajasiliamali’’

Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Mpanda Mohamed Masood amesema Benki hiyo imekuja na mpango na Huduma ya IMBEJU Kwa kutoa mikopo kwa vijana na wanawake wajasiliamli pasipo na Riba wala dhamana kwa masharti ya kuwa na biashara yeyote inayoonekana.

‘’hapa tunazungumzia IMBEJU maana yake ni mtaji wezeshi ambao utatolewa kwa wajasiliamali wadogo waliopo katika vikundi lakini haina maana kwamba tutatoa kwa kikundi tutatoa kwa mwanakikundi mmoja mmoja kwa sharti la kuwa mwanakikundi’’

Ameeleza kuwa utoaji wa mikopo hiyo kwa vijana na wanawake wajasiliamli utazingatia uhai wa Biashara inayofanyika  kulingana na mahitaji ya biashara husika kwa lengo la kuendelea kukuza biashara hiyo.

‘’Kama wewe ni Mfinyazi tutaangalia biashara yako hiyo kama wewe unatengeneza vikapu unauza matunda tutaangalia uwezo wako wa kufanya Biashara lakini ni kiasi gani biashara yako inataka ili iweze kukua’’ amesema Masoudy

Amebainisha kuwa kiwango cha mkopo kupitia IMBEJU kwa wanawake wajasiliamali utaanza kutolewa kuanzia shilingi Laki Mbili hadi Milioni Tano huku Vijana wajasilimali watakuwa na uwezo wa kukopa kuanzia kiasi cha Shilingi Lakimbili hadi Milioni Thelathini

Katika hatua nyingine amsema kuwa fursa hiyo itakuwa na uwezo kwa mnufaika kuwa na Akaunti maalumu ya Benki ya CRDB kwaajili ya Huduma hiyo ya IMBEJU

Monica Yusuph moja ya wanawake walishiriki katika hafla hiyo anasema ‘’tumeona kwamba mnatujali hata sisi wajasiliamali wadogo kupitia mikopo hii inaonyesha isahara ya kulijenga taifa kwa pamoja hongrereni sana CRDB Benki ‘’

Kwa upande wake Herena pascha amesema kuwa amefurahishwa na mpango huo wa CRDB benki kuja na Huduma ya IMBEJU itawasaidia kwakuwa haina Riba wala dhamana kwenye ukopaji wake.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages