MGANGA WA KIENYEJI MBARONI KWA KUTOROSHA NA KUISHI NA MWANAFUNZI KAMA MKE.

 

Na  Walter  Mguluchuma KTPC, Katavi 

Jeshi la Polisi Mkoa wa  Katavi  limefanikiwa kumkamata  Mganga wa Kienyeji  mmoja aitwaye  Mayala  Hinyali   mwenye  umri wa miaka 34 Mkazi wa Kijiji cha Kasekese Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi  baada ya kumtorosha S huleni  mwanafunzi wa kidato cha kwanza  mwenye umri wa miaka 16 jina limehifadhiwa  na kuishi nae kama mke wake .

Jeshi la Polisi Mkoa wa  Katavi  limefanikiwa kumkamata  Mganga wa Kienyeji  mmoja aitwaye  Mayala  Hinyali   mwenye  umri wa miaka 34 Mkazi wa Kijiji cha Kasekese Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi  baada ya kumtorosha S huleni  mwanafunzi wa kidato cha kwanza  mwenye umri wa miaka 16 jina limehifadhiwa  na kuishi nae kama mke wake .

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi  Benjamin Kuzaga alisema  mtuhumiwa huyo ambae anafanya shughuli ya Uganga wa kienyeji  alimtorosha mwanafunzi huyo wa shule ya Sekondari ya Usevya na kwenda kuishi nae kama mume na mke nyumbani kwake huko katika kijiji cha Kasekese .

 Mwanafunzi huyo alikuwa ni miongoni mwa wanafunzi waliojiunga na masomo ya kidato cha kwanza mwaka huu katika shule ya Sekondari Usevya Tarafa ya Mpimbwe Wilaya ya Mlele .

 Kamanda Kuzaga alieleza kuwa mtuhumiwa huyo baada ya kumtorosha mwanafunzi huyo  alimtowa kwenye  Shule  hiyo na kumsafirisha hadi kwenye Kijiji cha Kasekese ambako  alikuwa akiishi na kuanza kuishi  nae kama  kama mke wake bila kujari kuwa  msichana huyo nado ni mwanafunzi na haja fikia umri wa kuolewa .

 Alisema jeshi la Polisi lilipata taarifa za Mganga huyo wa kienyeji juu ya kumtorosha  mwanafunzi huyo kutoka kwenye shule aliyokuwa ameanza kusoma na kwenda kuishi nae akiwa mke wake .

 Kufutia taarifa hiyo jeshi hilo lilianza kufanya msako  kwa kushirikiana na uongozi wa Kijiji cha Kasekese wa kumsaka mtuhumiwa huyo  Mayala  Hinyali na ndipo walipo weza kufanikiwa kumkamata mtuhumiwa  akiwa nyumbani kwake akiwa akiishi na mwanafunzi huyo  mwenye umri mdogo wa kidato cha kwanza .

 Kamanda Kuzaga alisema kuwa mtuhumiwa huyo bado anaendelea kushikiliwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi  ili aweze kufikishwa Mahakamani kwa hatua za kisheria zaidi ili iwe  fundisho na kwa watu wengine wenye tabia kama hiyo ya kukatisha ndoto za wanafunzi wa kike kumaliza masomo yao  kwani kwenye Mkoa wa Katavi matukio kama hayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara.

 Katika hatua  nyingine  jeshi la  Polisi  Mkoa wa Katavi limefanya msako mkali wa kuwasaka wezi wa pikipiki kufatia wimbi kubwa lililokuwa limeenea katika Mkoa wa Katavi na katika msako huo wamefanikiwa  kukamata jumla ya pikipiki  kumi na mbili ambazo zilikuwa zimeibiwa  na watuhumiwa kumi na  tano  wamekamatwa kwenye msako huo na wanashikiliwa na jeshi la Polisi .



 Kamanda     Benjamin Kuzaga  aliwaambia Wandishi wa Habari kuwa watuhumiwa hao walikamatwa hapo  machi tatu katika maeneo tofauti tofauti baada ya jeshi la Polisi kuwa limegundua mtandao wa watu wanaojihusisha na wizi wa pikipiki .

 Alisema   kuwa wahalifu hao baada ya kuwa wamefanikiwa kuiba pikipiki wamekuwa  wakifuta chesesi  namba pamoja na namba za injini  ili zisiwe rahisi kugundulika kwa  wenye umiliki wa pikipiki wanazokuwa wameziiba

 Vielelezo hivyo vya pikipiki   vipo katika kituo cha polisi cha Wilaya ya Mpanda na watuhumiwa  wote bado wanaendelea kushikiliwa na polisi na mara upelezi utakapo kamilika watafikishwa Mahakamani ili wakajibu tuhuma zinazo wakabili .

 Kamanda Kuzaga ametowa wito kwa wananchi kufika kwenye kituo cha Polisi cha Mpanda Mjini ili waweze kuzitambua pikipiki zao zilizo ibiwa  na wafike wakiwa na nyaraka  halali ambazo  zinazowathibisha kuwa wao ndio wamiliki halali wa mali hizo


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages