LATCU YAPIGA MARUFUKU NGULAI KWENYE TUMBAKU.

Meneja wa Chama kikuu cha ushirika Latcu Mkoa wa Katavi Pius Kilo akizungumnza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa 32 uliofanyika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda

Na Mwandishi wetu-Katavi

Wakulima wa zao la Tumbaku katika Mkoa wa Katavi wameonywa kuacha tabia ya kuchanganya vitu visivyo faa kwenye zao la Tumbaku kwa lengo la kuongeza uzito wa zao hilo wakati wa Masoko.

Wakulima wa zao la Tumbaku katika Mkoa wa Katavi wameonywa kuacha tabia ya kuchanganya vitu visivyo faa kwenye zao la Tumbaku kwa lengo la kuongeza uzito wa zao hilo wakati wa Masoko

Agizo hilo limetolewa na Meneja wa Chama kikuu cha Ushirika Mkoa wa Katavi LATCU Pius Kilo wakati wa mkutano mkuu wa 32 mwaka uliofanyika katika ukumbi wa Manispaa ya Mpanda.

Amesema kuna baadhi ya wakulima wamekuwa wakichanganya Vitu visivyo faa kwenye zao la Tumbaku hali ambayo imekuwa ikipelekea kutaka kuharibu soko la Tumbaku kwa wakulima wa Mkoa wa Katavi na Tanzania kwa ujumla.

Froria Haule Mkurugenzi wa Maendeleo ya ushirika shirikisho la vyama vya ushirika Tanzania akitoa neno kwenye mkutano Mkuu wa 32 wa Chama kikuu cha Ushirika Latcu Mkoa wa Katavi
Ameeleza kuwa baadhi ya Makampuni ya ununuzi wa Tumbaku yamekuja na minyororo na mawe ambayo yamekutwa yamechanganywa na wakulima kwenye zao la Tumbaku kinyume na sheria zinazosimamia zao hilo.

Katika hatua nyingine amesema zao la Tumbaku nimiongoni mwa mazao yanayoipatia nchi fedha za kigeni ambazo husaidia ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya maendeleo kwa wanannchi huku akisistiza wakulimakujiepusha kuchanganya ngulai kwenye Tumbaku zao wakati wa Masoko.

Kwa upande wake Frorian Haule Mkurugenzi wa maendeleo ya ushirika shirikisho la vyama vya ushirika Tanzania amesema kumekuwa na Tabia kwa baadhi ya wakulima kuchanganya Tumbaku na vitu visivyofaa kwa lengo la kujiongezea kipato hali ambayo hushusha hadhi biashara ya zao hilo.

Ametoa wito kwa viongozi wa vyama vya Amcos kwenda kusimamia ubora wa zao hilo bila kufanya uchafuzi wa aina yeyote ile kwakuwa kufanya hivyo kunazidi kupunguza sifa kwa wanunuzi wa ndani na wanunuzi wanje. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages