BALOZI WA UTALII AWAOMBA WANANCHI KATAVI KUTEMBELEA VIVUTIO VYA UTALII

Balozi wa Utalii hapa nchini Nangasu Warema akiongea na wadau wa Utalii mkoa wa Katavi katika kongamano la utalii lililofanyika mkoa wa Katavi.


Na Paul Mathias-Katavi

Wananchi katika mkoa wa Katavi wameobwa kujenga utamaduni wa Kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi kama sehemu ya uzalendo na kukuza utalii wa ndani.

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Onesmo Buswelu akimwakilisha mkuu wa Mkoa wa Katavi katika kongamano hilo

Wananchi katika mkoa wa Katavi wameobwa kujenga utamaduni wa Kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi kama sehemu ya uzalendo na kukuza utalii wa ndani.

Hayo yamebainishwa na Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Onesmo Buswelu wakati akiwa hutubia wadau wa Utalii katika Kongamano la Kampeni ya Utalii na Mama Samia Hifadhi ya Taifa ya Katavi lililofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Bwalo la Polisi Mpnda Mjini.

Wadau mbalimbali wa utalii wakiwa katika kongamano la utalii katika ukumbi wa Bwalo la Polisi Mpanda Mjini

Buswelu amesema kuwa wananchi katika Mkoa wa Katavi wanayofahari ya kujivunia uwepo wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi pamoja na kuwasehemu ya utalii kwa kutembelea hifadhi hiyo ili kukuza uchumi wa mkoa wa Katavi kupitia utalii wa ndani.

‘’Tupende kuthamini vya kwetu na wengine watavipa thamani kubwa tukivichukia vya kwetu hayupo atakakae kuja kuvipenda vya kwetu tuipende mbuga yetu ya Katavi kwa kuitembelea na kwenda kujionea wanyama mbalimbali’’amesema Buswelu.

Ameeleza kuwa kutalii kunafaida ikiwemo kupunguza mawazo na kuongeza utimamu wa akili katika kukabiliana na Majukumu ya Kila siku .

’'Kutalii kunaongeza utimamu wa akili unakuwa na Maisha Mapya kwa wakati huo twende tukatalii tuwahimize watu tuhamasishe waje kutalii”amesisitiza Buswelu

Kwa upande wake Balozi wa Utalii Tanzania aliyekuwa Mgeni Mwalikwa  katika Kongamano hilo Nangasu Warema amesema kuwa kupitia utalii kunaongeza vipato vya uchumi kwa wananachi wa mkoa wa Katavi na kuawasa wananachi kutembelea hifadhi ya Taifa Katavi.

‘’Watalii watakapokuja Mpanda watawekeza Mama Ntilie atapata hela,Nyumba za kulala Wageni zitapata hela lakini pia kule hifadhini Mapato yataongezeka na taifa litaingiza Pesa amesema Warema’’

Amesema kama Balozi wa Utalii hapa nchini amekuwa akitembea mikoa mbalimbali hapanchini kwa lengo la kuhamasisha utalii na kwa lengo la kuhakikisha wananachi na wadau wa utalii hapa nchini wanakuwa mabalozi wazuri kuhusu utalii kwa kutenbelea vivutio vya utalii.

‘’Nimekuwa nikitembelea maeneo mbalimbali katika Mikoa ya kusini na Magharibi Kushirikiana na wadau na watu wa Sekta ya Utalii ikiwemo Tanapa’Ameeleza Warema.

Thomas Ngozi mmoja wa Washiriki katika Kongamano hilo amesema wakati umefika sasa kwa serikali ya Mkoa wa Katavi kupitia mamlaka zinazo husika kuendeleza maeneo mbalimbali ya uhifadhi na mali kale zilizopo mkoa wa Katavi ili kizazi Kijacho kiwe sehemu ya wanufaika na utalii.

‘’Mkoa huu unavivutio vingi vya utalii mfano kuna mlima wa Lyambalya Mfipa maeneo haya yakitunzwa na kutangazwa yatakuwa na tija katika vizazi vijavyo anasema Thomas Ngozi’

Kwa upande wake Teddy Kapufi mmoja ya washiriki wa Kongamano hilo ameomba gharama za kuingia katika hifadhi ya Taifa ya Katavi ikiwa ni sehemu ya kuvutia makundi yenye kipato cha chini kutembelea hifadhi hiyo hususani wakazi wa mkoa wa Katavi.

Kongamano hilo la Kampeni ya Utalii na Mama Samia Hifadhi ya Taifa ya Katavi limehudhuliwa na wadau mbalimbali wa utalii katika mkoa wa Katavi likiwa na lengo la kuchochea na kukuza utalii kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi na Tanzania kwa ujumla.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages