WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MPIMBWE WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA WIZI WA BILIONI 1.2


watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe wanaotuhumiwa kwa wizi wa  fedha Shilingi Bilioni 1.2 wakiwa chini ya ulinzi wa maafisa wa Takukuru walipofikishwa Mahakama ya hakimu mkazi Katavi kabla ya Kusomewa Mashitaka.


Na Walter Mguluchuma,Katavi

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa  Mkoa wa Katavi imewafikisha   Mahakamani watumishi  saba wa Halmashauri ya  Wilaya ya  Mpimbwe  Mkoani  Katavi  akiwemo  mtunza  hazina wa Halmashauri hiyo kwa kutuma za wizi wa zaidi ya  shilingi Bilioni 1.2 walizokuwa wakiziingiza kwenye  akaunti za watu binafsi .

Watumishi wa Halmashauri ya Mpimbwe wakiwa wanaingia katika jengo la Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Katavi chini ya ulinzi wa Maofisa wa Takukuru


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa  Mkoa wa Katavi imewafikisha   Mahakamani watumishi  saba wa Halmashauri ya  Wilaya ya  Mpibwe Mkoani  Katavi  akiwemo  mtunza  hazina wa Halmashauri hiyo kwa kutuma za wizi wa zaidi ya  shilingi Bilioni 1.2 walizokuwa wakiziingiza kwenye  akaunti za watu binafsi .

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Faustine  Maijo  amewataja watuhumiwa hao waliofikishwa  Kizimbani na  Takukuru Mkoa wa Katavi kuwa ni  Canuthe Matsindiko, Michael Katanga(Big),Masami  Mashauri ambae  ni mweka   hazina wa  Halmashauri hiyo(DT) Tumaini  Misese,Maila  Oluomba , Emanuel  Salanga  na  Laurent  Sunga.

Maijo  alisema  watuhumiwa hao wamefikishwa  Mahakamani na  kusomewa   mashitaka  katika  Mahakama ya  Hakimu   Mkazi    Katavi na kusomewa  mashitaka na    mbele ya  Hakimu    Mfawidhi wa  Mahakama  hiyo  Gwai  Sumai

Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi,Faustine Maijo akieleza mbele ya waandishi wa Habari juu ya  kufikishwa Mahakamani kwa watuhumiwa saba wa Halmashauri ya Mpimbwe.

Amesema kuwa watuhumiwa hao saba  kati yao  watumishi wa  Halmashauri ya  Mpimbwe ni watano   na mmoja na  wamanispaa ya  Mpanda na  mwingine alikuwa ofisi ya Mkuu wa  Mkoa wa Katavi kwa sasa yupo Shirika la  masoko  Kaliakoo.

Amebainisha   kuwa  kabla ya  kukamatwa kwa watumishi hao Takukuru  Mkoa wa Katavi walipokea taarifa juu ya  ubadilifu wa fedha katika Halmashauri ya  Mpimbwe  ulikuwa ukihusu wizi wa fedha kiasi cha Tshs  1,232 869,000  fedha hizo zikuwa  kwenye  akaunti ya Halmashauri ya   Mpimbwe na walizifuja kwa kusingizia kuwa  waliwalipa wakandarasi  ambao walifanya shughuli mbalimbali jambo ambalo  halikuwa na ukweli .

Maijo  alisema  uchunguzi waliofanya wamebaini  fedha hizo walizilipa kwa watu binafsi  ambao hawakuwa na kazi yoyote  walizofanya katika Halmashauri hiyo  lakini waliwalipa watu ambao walikuwa wakifahamiana nao  kwa kibali kuwa wamewalipa wakandarasi waliokuwa wakifanya kazi za ukandarasi mbalimbali .

Watumishi hao wamefikishwa Mahakamani na kusomewa mashita matatu  shitaka la kwanza  wameshitakiwa kujihusisha na genge la uhalifu  shitaka la pili ni la  uhujumu  uchumi na shitaka la tatu ni  wizi .

Mwendesha mashitaka  wa  Takukuru  Mkoa wa Katavi  Kelvin  Mwaja  alisema wamewafungulia mashita watuhumiwa hao wote saba kesi namba tano ya uhujumu uchumi ya  2023 katika Mahakama ya Hakimu ya   Mkazi  Katavi.

 Washitakiwa hao kwa pamoja wameshitakiwa kwa makosa ya uhujumu uchumi kinyume cha aya ya nne  [c ]na kifungu cha 57(1)  60 (  2  ) cha sheria ya uhujumu uchumi  sura ya  200   marejeo ya  2022 washitakiwa hao  wote wanadaiwa kama watumishi wa Halmashauri hiyo  kwa pamoja waliunda genge la uhalifu  kwa lengo la kujipatia manufaa  walifanya matukio kwa  mtililiko kwa lengo la kufanana  na kujipatia manufaa ya kiasi hicho cha fedha .

Shitaka la pili wanashitakiwa  washitakiwa kwa kosa la  kuisabishia   Halmashauri hasara kinyume na kosa la kifungu cha sheria  sura ya 10(1) na  57 [1] na 60[2] sura ya 200 Marejeo ya 2022

Kosa la taui ni wizi  ambalo wameshitakiwa  kinyume na kifungu cha sheria  namba   265 na 270  kinyume  na kifungu    kanuni ya adhabu sura  marejeo ya 2022 kwa pamoja wanadaiwa kuiba kiasi cha shilingi Bilioni  1.2 kwa kuwa ni watumishi wamekiuka kifungo cha sheria namba 270 kwa kufanya wizi wakiwa watumishi wa umma .

 Watuhumiwa hao baada ya kusomewa mashita  waliambiwa na  Mahakama kuwa hawatakiwi kujibu lolote kwa kuwa Mahakama  hiyo ya Hakimu Mkazi  Katavi  haina  mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ya uhujumu uchumi mpaka mahakama ya juu zaidi ya hiyo .

Hakimu  Mfawidhi  wa Mahakama ya Mkoa wa Katavi Gwai Sumai alihairisha kesi hiyo hadi hapo septemba 4 na watuhumiwa hao wote saba waliamriwa kwenda     katika  gereza la   mahabusu la   Mpanda  mjini  hadi hapo siku ya tarehe hiyo

Kwa habari zaidi endelea kutembelea ukurasa wetu wa

kataviclub.blogspot.com

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages