ASHIKILIWA NA POLISI KWA TUHUMA ZA KUMUUA MKEWE KWA KUNYIMWA TENDO LA NDOA

 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi,Kaster Ngonyani 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia  Busu  Lugwisha(51) mkazi wa Kijiji cha Masigo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumuua mke wake aitwaye  Regina  Thobias (40)  kwa kumpiga na kitu  kizito chenye mcha kali  kichwani  baada ya  kunyimwa  tendo la ndoa na mkewe kwa muda  mrefu.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi linamshikilia  Busu  Lugwisha(51) mkazi wa Kijiji cha Masigo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi kwa tuhuma za kumuua mke wake aitwaye  Regina  Thobias (40)  kwa kumpiga na kitu  kizito chenye mcha kali  kichwani  baada ya  kunyimwa  tendo la ndoa na mkewe kwa muda  mrefu.

Kamanda wa polisi wa Mkoa wa  Katavi Kaster Ngonyani amesema  tukio   hilo  la mauaji hayo ya kusikikisha limetokea  Februari  19  majira ya saa kumi usiku nyumbani kwa wanandoa hao wawili waliokuwa wakiishi wakiwa mume na mke .

Kamanda  Ngonyani amesema   chanzo cha mauaji hayo  ya mwanamke huyo  kilitokana na wivu wa mapenzi  kwa kile kunachodaiwa ni  hasira zamthumiwabaada yakunyimwa tendola ndoa na  Ragina  Thobias ambae alikuwa ni mke wake .

 Amefafanua kuwa  kutokana na wivu huo wapenzi ndio ulimfanya mtuhumiwa  Busu  kumpiga  kichwani  na kitu kizito  kichwani  upande  wa  kisogoni  na kumsababishia  mkewe  kufa hapo hapo .

Ameeleza kuwa katika mahojiano ya awali na mtuhumiwa   jeshi la polisi limebaini  mauaji hayo  yametokana na wivu  wa mapenzi baada ya mtuhumiwa kukiri kufanya mauaji hayo kwa kile alichodai kuwa mkewe alikuwa amenyima  tendo la ndoa kwa muda mrefu sasa .

Mwili wa marehemu  umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti katika kituo cha afya  cha Inyonga B kwa ajiri ya uchunguzi zaidi na mara uchunguzi utakapokuwa umekamilika watakabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya mazishi .

Kamanda  Ngonyani amesema mtuhumiwa  bado  anaendelea kushikiliwa  na polisi na mara upelelezi ukikamilika atafikishwa mara moja mahakamani ili akajibu tuhuma zinazo mkabili .

Jeshi la Polisi linatowa wito watu waache tabia  ya  kujichukulia sheria  mikononi  na  badala yake  wawasilishe  changamoto  zinazowakabili kwa  viongozi wao wa familia dini  mitaa  au mamlaka  za kisheria  kwa ajiri  ya utatuzi .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages