WANANCHI WAMUOMBA AMRI JESHI MKUU KUTATUA MGOGORO WA ARDHI KATAVI.

                           

Na  Walter Mguluchuma KTPC,Katavi

Zaidi y a  Kaya 100O   katika Manispaa ya  Mpanda  Mkoani Katavi wanaolima mazao yao kwenye eneo la Kampuni wamemwomba amiri jeshi Mkuu wa  Majeshi ya Tanzania  Samia  Suluhu Hassan  kuweza kutatua  kutatua mgogoro wao wa  ardhi na jeshi la wananchi ulidumu kwa kipindi cha muda mrefu sasa pasipokupatiwa ufumbuzi.


Zaidi y a  Kaya 100O   katika Manispaa ya  Mpanda  Mkoani Katavi wanaolima mazao yao kwenye eneo la Kampuni wamemwomba amiri jeshi Mkuu wa  Majeshi ya Tanzania  Samia  Suluhu Hassan  kuweza kutatua  kutatua mgogoro wao wa  ardhi na jeshi la wananchi ulidumu kwa kipindi cha muda mrefu sasa pasipokupatiwa ufumbuzi.

Maombi hayo  ya wananchi hao yametolewa hapo leo na wananchi hao waliokuwa wamekusanyika katika ofisi ya CCM Mkoa wa Katavi  kwa lengo la kufikisha kilio chao .

Thomas  Jeremia  mmoja wa wananchi hao ambae ndie wahanga wa eneo hilo maarufu kwa jina la Kampuni   alisema kuna jumla ya Kaya 1,100 ambazo zimeathiri katika mgogoro huo wa ardhi .

Amesema kuwa kuna watu tisa waliwahi kuvunjwa miguu na kulazwa hospitalini mwaka jana baada ya kupokea kipigo na wengine wamekuwa wakichomewa  nyumba zao.

Hivyo wanamuomba    Amiri  jeshi Mkuu wa Majeshi ya Tanzania  aweze kuwasaidia kutatua mgogoro huu ili wananchi waweze kupatiwa haki yao .

 Amebainisha kuwa eneo hilo lina ukubwa wa ekari zaidi  ya ekari 2000.

 Zeno  Kamsonki   alisema kuwa mbaya zaidi  wananchi hao ambao hapo  walikuwa wanamiliki maeneo hayo wala hawaja wahi kulipwa fidia yoyote endapo kama jeshi la wananchi kama wangekuwa wanahitaji kumiliki eneo hilo kama ambavyo sheria zinazoelekeza .

Brijita  Pascal alisema kuwa yeye ni mjane na alikuwa amelima mahindi mwaka huu na wanajeshi la wananchi walifyeka   mahindi yake zaidi ya ekari mbili hari ambayo itamfanya mwaka huu ataishi kwa shida .

 Ameeleza kuwa Askari hao pia wamekuwa na tabia ya kuwapiga wananchi na hata yeye mtoto wake mmoja alipigwa na kuvunjwa mguu.

 Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Katavi Beda Katani aliwaeleza wananchi kuwa chama kimesikia  malalamiko hayo .

Amesema wao kama chama swala hilo  wameisha lipokea  muda mrefu  na wanasubiri maamuzi ya kutoka ngazi za juu juu ya  mgogoro huo.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages