TAKUKURU  KATAVI  WAOKOA  ZAIDI YA MILIONI 34 NA NG`0MBE  6 ZILIZOTOLEWA  BAADA YA MTU KUBAMBIKIWA KESI YA MAUAJI

 

Na  Walter Mguluchuma, Katavi

Taasisi ya  Kuzuia na Kupambana  na Rushwa (TAKUKURU )Mkoa wa Katavi imefanikiwa kuokoa kiasi cha zaidi ya  shilingi milioni 34 na ng`ombe 6 kupitia  kazi walizofanya za uzuiaji wa Rushwa  kati ya fedha hizo   Tsh 28,258,040.00 zimeokolewa Halmashauri ya Mlele  ikiwa ni fedha  zilizofanyiwa ubadilifu na na baadhi  ya watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele .

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Sipha  Mwanjala  wakati akitowa taarifa  mbele ya vyombo vya Habari  juu  ya utendaji kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu ya kuanzia  Januari  hadi Machi .

Mwanjala amesema  wameweza kusaidia  kuokoa kiasi cha tsh  34,851,040 pamoja na Ng`ombe 6 kupitia  kazi ya uzuiaji wa Rushwa  na uchunguzi  hali  iliyofanya  kuongezeka kwa mapato  katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele

Amefanua kuwa  sh ,28,258,040.00 zimerejeshwa  katika akaunti  ya Halmashauri ya Wilaya ya Mlele  ikiwa ni fedha ambazo zilifanyiwa ubadilifu  na baadhi ya watumishi  waliokusanya ushuru  kupitia mashine  za  POS   na baada ya kuzikusanya fedha hizo  hawakuziwakilisha benki  kama ambavyo  inatakiwa .

Ng`ombe  6  pamoja na  sh 1,700,000  zimerejeshwa  kwa  kwa mwananchi  ambae  alikuwa amezitowa  kama faini baada ya  kusingiziwa kesi  ya mauaji  na Askari  Polisi    aliyeshirikiana na wananchi  wawili pia  sh 3,184,000 zimerejeshwa  katika kitongoji cha  Mbongwe Wilaya ya Tanganyika  kufatia  baadhi ya viongozi  na Sungusungu  kugawana  fedha   za kutoka kwa wananchi walizochanga za ujenzi wa shule ya Msingi.

Kuhusu ufatilaji wa miradi ya  maendeleo Takukuru Mkoa wa  Katavi  imeweza kufatilia  miradi ya Maendeleo  22 yenye thamani  kiasi cha  shilingi Bilioni  14.8 kwenye sekta za  Elimu ,Afya, uchumi , na miundombinu  ili  kuweza kubaini  viashiria  vinavyoweza  kusababisha  upotevu  wa rasilimali za umma .

Mwanjala amesema  katika kipindi hicho wamepokea malalamiko  64 yliyohusiana  na tuhuma za Rushwa  na uchunguzi ulifanyika  na  kubaini malalamiko 26  hayakuwa yanahusiana na  tuhuma za  Rushwa  hivyo walalamikaji  walisaidiwa na kushauriwa  sehemu sahihi za kupeleka malalamiko yao

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages