WANANCHI KATAVI WALIA NA WATOTO  KUUZA VYUMA CHAKAVU  NA CHUPA ZA PLASITKI


Na  Wandishi wetu  Katavi

Baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamelalamikia kuwepo kwa ongezeko kubwa  la watoto  wanao  zurula mitaani muda wa masomo   huku wakipita kwenye nyumba za watu  na kubeba vyuma  vya aina mbalimbali pamoja masafulia ,ndoo za plasitiki  na kwenda kuuza kwenye maaneo yanayonunua vyuma chakavu .

 Humud  Juma  Mkazi wa Mtaa wa Majengo  Manispaa ya Mpanda amesema changamoto hiyo imekuwa  ni kubwa sana kwa watoto wanao pita mitaani  tena wakati wa masomo  na kufafuta  vyuma  chakavu ndoo za plasitiki   na safulia ,

Samome John  amebainisha kuwa  imekuwa  shida sana kwa watu wenye nyumba ambazo  hazina uzio  kwani ukiacha  nje kidogo tuu vyombo  vyako vya bati au ndoo zaaina zote unakuta wamebaba .

Ameomba mamlaka  zinazohusika  kuangalia namna ya  kuondoo tatizo hilo la watoto  wangepiga hata  marufuku kwa wanao nunua  vyuma chakavu na  vitu vya plastiki  kutofanya  biashara ya  na watoto  na endapo hali hii itaendelea  upo uwezekana wa kuzalisha  watoto wakao kuwa  wahalifu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages