Na Walter Mguluchuma
Katavi
Mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania Kanda ya Magharibi kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi vya Mkoa wa Katavi wamefanya zoezi la utayari wa ukoaji wa ajari ya ndege pindi ajari itakapo kuwa imetokea kwa mafanikio makubwa
Kamanda wa Polisi wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kaster Ngonyani amesema zoezi hilo linawajengea uwezo mkubwa sana endapo itakapokuwa ajari ya ndege imetokea kwa kuweza kufika kwa haraka sana kwenye eneo la tukio kama walivofanya kwenye zoezi hilo kwa bidii wakiwa na wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Mpanda .
Amesisitiza kuwa hilo lilofanyika ni zoezi tuu sio kwamba kuna ajari ya ndege ambayo imeanguka kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda bali ni zoezi tuu la utayari
Kaimu Kamanda wa jeshi la zima moto na uokoaji wa Mkoa wa Katavi Liliana Joshuwana amesema walikuwa katika uwanja wa ndege wa Mpanda kwa ajiri ya zoezi la utayari kwa ajiri ya ndege iliyodondoka Ikiwa na abiria 30 lakini hamna kifo kilichotokea wote walikuwa majeruhi zoezi hilo sio kwamba ndege ilikuwa imeanguka kiuwalisia ni zoezi la utayari kwa vyombo vyote vya ulinzi na usalama .
Amewatowa hofu wananchi wa Mkoa wa Katavi na Wanzania kuwa hilo likuwa ni zoezi la utayari wa uokoaji na sio ajari ya ndege kiuhalisia .
Meneja wa viwanja vya ndege Kanda ya Magharibi Fadhili Maginema amebainisha kuwa wafanya zoezi la utayari wa ajari ya ndege kama ambavyo matakwa ya kisheria na kikanuni ya mdhibiti wa mamlaka ya anga Tanzania ambayo inawahitaji wafanye zoezi hilo la utayari kila baada ya miaka miwili .
Amefafanua kuwa zoezi hilo limehusisha taasisi zote ambazo zipo kwenye maokozi yaani Polisi ,jeshi la zima moto , Jeshi la wananchi wa Tanzania , usalama wa Taifa na Mahospitali yote yaliyokatika Mkoa wa Katavi na mamlaka ya viwanja vya ndege wanachoangali ni namna ya kujilinda wakati wa ajari kwa kila taasisi kujua wajibu wao wanaotakiwa kufanya pindi ajari ikitokea .


