UWT MPANDA WATOA MSAADA KWA WANAFUNZI WENYEMAHITAJI MAALUMU.



Katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Katavi Asha Juma (wa pili kushoto) akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa tatu kulia,Abel Kimanzi walipokuwa wakitoa mahitaji kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu wa Shule ya Msingi Azimio.


Na Mwandishi Wetu KTPC,Mpanda.

Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wamewatembelea wanafunzi  wenye uhitaji maalumu na kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali ya kujikimu pamoja na kuwatia hamasa ya kusoma kwa bidii.

Hayo yamefanyika kuelekea maadhimisho ya kutimiza miaka 44 ya ccm ambapo walitembelea shule ya msingi Azimio na shule ya sekondari Rungwa zilizopo manispaa ya Mpanda Mkoani hapa.

Katibu wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Manispaa ya Mpanda,Azizia Self (wa tatu kushoto) akitoa dumu la mafuta ya kula kwa shule ya Msingi Azimio manispaa hapo yenye watoto wenye mahitaji maalumu.

Mwenyekiti wa UWT Mkoa  wa Katavi Fuljensia Kapama akikabidhi jana vifaa hivyo kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Msingi Azimio amesema kuwa wamewapatia Mchele,Mafuta ya kupikia na majani ya chai vyenye thamani ya 180,000/-sambamba na gunia moja la mahidi na vifaa vya darasani karamu na daftari vyote vikiwa na thamanii ya 200,000/-

Fuljensia ameleza kuwa kama wanawake wameona kunaumuhimu mkubwa wa kuwasaidia wanafunzi hao kwa sababu ni sehemu ya jamii ambayo inapaswa kuhudumiwa kwa kila kitu ili kufanikisha ndoto za wanafunzi hao.


Mwalimu wa Mkuu wa Kitengo wa wanafunzi wenye ulemavu wa shule ya msingi Azimio Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi Mwl Joseph Fortunstus ( suti nyeupe) akiongea kwa lugha ya alama wakati akieleza jambo mbele ya viongozi  wa UWT.

‘’ naiomba jamii ya mkoa wa Katavi kutambua kuwa inawajibu wa kuhakikisha watoto ambao ni  walemavu wote wanapatiwa haki ya kupewa elimu…kuwaficha watoto wenye ulemavu ni kitendo kimepitwa na wakati hivyo tuwapeleka na tujitolee kuwa hudumia kila wakati’’ alisema Mwenyekiti huyo.

Mwl Joseph Fortunatus,Mkuu wa kitengo cha wanafunzi wenye uhitaji maalumu katika shule ya msingi Azimio,Akipokea mahitaji hayo licha ya kuishukuru UWT pia ameishukuru serikali kwa kuendelea kuwahudumia wanafunzi hao kwa kuwapatia chakula bure.

Aidha alisema kuwa bado wanakabiliwa na changamoto ya uhaba wa walimu,uchache wa vifaa  vya kufundishia  wanafunzi wenye mahitaji maalumu,Uhaba wa vyumba vya madarasa pamoja na kukosekana kwa jiko la kupitia chakula.

Baaadhi ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu wa shule ya msingi Azimio Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi

Aisha Juma,Katibu wa UWT Mkoa wa Katavi amesema licha ya kutoa mahitaji hayo na kukubali kushughurikia baadhi ya changamoto hizo kwa kuishauri serikali kufanya maboresho kwenye shule hiyo pia alisema wataendelea zaidi kuhamasisha na taasisi zingine ili kusaidia wanafunzi hao.

Vilevile Katibu huyo amesema kuwa wamefanikiwa kutoa elimu ya afya ya uzazi kwa wanafunzi wa sekondari Rugwa ili kuwawezesha kujitambua na kuepukana na mimba za utotoni ambazo kwa kiasi kikubwa zimeshuhudiwa mkoani Katavi.

Katibu huyo amesema kuwa ni jambo ambalo haipendezi kwa mkoa kushika nafasi za juu kwenye mimba za utotoni,Hivyo kama UWT wanawajibu wa kuwapa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wote  pamoja na kuwahimiza wazazi na walezi kusimama kwenye nafasi zao za kuwalinda watoto dhidi ya mimba ambazo zinauwa ndoto zao.


Wanafunzi wa jinsi ya kike wa shule ya sekondari Rungwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wakiwa katika hali ya utuliwa wakati wa mafunzo maalumu ya siku moja ya elimu ya afya ya uzazi ambapo wamehimizwa na UWT Mkoa wa Katavi kujikinga na mimba za utotoni.

Awali ya hayo Katibu wa  UWT Manispaa ya Mpanda ,Aziza Seif akisoma taarifa kwa waadishi wa habari ya kuelekea maadhimisho ya miaka 44 ya CCM amesema kuwa wamefanikiwa kufanya huduma za afya ili kujikinga na magonjwa yasiyo ya kuambukizwa kama vile kisukari,uzito ,mapigo ya moyo,kutoa elimu ya saratani na upimaji wake kwa wanawake pamoja na elimu lishe.

UWT katika maadhimisho hayo wameandaa huduma ya utowaji wa damu kwa kushirikiana na wataalamu wa huduma ya afya kutoka hosptali ya rufaa Mkoa wa Katavi.

Mwenyekiti wa Chama Chama Mapinduzi Wilaya ya Mpanda Abel Kimanzi (wa tatu kulia) akikabidhi gunia la mahidi mwanafunzi wa shule ya Sekondari Rungwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Rehema Mansoul(tatu kushoto)


Mwanafunzi wa Kidato cha tatu Aisha Hassin shule ya sekondari Rungwa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi akipongeza UWT kwa kuwatembelea shuleni hapo.



Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages