UDESO WAJA NA MRADI KUFATILIA TAARIFA ZA CAG.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Usevya Development Eden Wayimba akifungua mafunzo kwa wajumbe wa kamati za Pets kutoka vijiji vya Lugonesi na Kasekese.

Na Waltre Mguluchuma.

Katavi

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Usevya  Development Sociaety(UDESO) imeanza kutekeleza mradi wa Audit Accountability  Initiative(AAI) katika Wilya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi ukiwa na lengo la kuangalia  utekelezaji  wa mapendekezo  yaliyotolewa katika Sekta ya Elimu ya msingi na awali  kupitia ripoti iliyotolewa na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG).

Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Usevya  Development Sociaety(UDESO) imeanza kutekeleza mradi wa Audit Accountability  Initiative(AAI) katika Wilya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi ukiwa na lengo la kuangalia  utekelezaji  wa mapendekezo  yaliyotolewa katika Sekta ya Elimu ya msingi na awali  kupitia ripoti iliyotolewa na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali (CAG). 

Hayoyamesemwa na  Mkurugenzi Mtendaji  wa Usevya Development Society  Eden Wanyimba  wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa  mafunzo ya  siku tano ya  kuwajengea uwezo  wajumbe wa kamati  za PETS  wa  kutoka katika Vijiji  viwili  vya lugonesi na  Kasekese  yatakayo wawezesha  kufanya majukumu yao  kwa ufasaha  watakayopangiwa  katika muendelezo  wa utekelezaji wa   wa radi huu[ AAI]

Mafunzo hayo   yatawawezesha kubaini  vikwazo  mbalimbali  vinavyiikumba  miradi  ya maendeleo katika Vijiji vyao  na kushauri namna bora  ya kufanya  ili  kuifanya miradi  ya maendeleo  katika jamii zao  kwa ufanisi  wa hali ya juu.

Washiriki mbalimbali katika semina ya Wajumbe wa Pets katika kutoka Vijiji vya Kasekese wakiwa katika picha ya Pamoja na mkurugenzi wa taasisi isiyokuwa ya kiserikali ya Usevya Development Society[UDESO]

 Wayimba amebainisha kuwa  Udeso  kwa kushirikiana na  Taasisi  ya WAJIBU  Insitute  of public Accountability Initiative [AAI] Katika wilaya ya Tanganyika  hususani katika vijiji vya Lugonesi na Kasekese  ambao ulianza kutekelezwa tangu Mwezi March 2023 na utamalizika Mwezi Agust Mwaka huu.

Amefafanua kuwa Mwezi March Mwaka huu walitambulisha Mradi kwa ngazi tofauti tofauti kuanzia ngazi za Vijiji ambavyo Mradi huu unatekelezwa baada ya utambulisho huo kamati za Pets kutoka katika vijiji hivyo viliundwa kupitia serikali zao za mitaa na wanavijiji wa Vijiji vya Lugonesi na Kasekese zikiwa na wajumbe 10 wanawake Watano na wanaume Watano.

Amesema mbali ya Mradi huu UDESO imekuwa ikiwezesha Maendeleo ya Jamii Katika sekta Mbalimbali kwa kushirikiana na wadau tofautitofauti miongoni mwa sekta ambazo UDESO wameshirikiana nazo nipamoja na Sekta ya Afya,Elimu,Mazingira,Maendeleo ya Jamii Jinsia wazee na watoto,Kilimo,na Technolojia ya habari na Mawasiliano.

Washiriki wa Mafunzo ya kamati za Pets wakiwa katika Semina hiyo.

Wayimba ameeleza kuwa Taasisi ya UDESO tangua kuanzishwa kwake 2005 imeweza kushiriki na kukuza Maendeleo ya Mkoa wa Katavi na Taifa kwa ujumla kwa kutekeleza miradi Mbalimbali kwa kushilikiana na Serikali.

Elizia Feston Mjumbe wa Pests kutoka kijiji cha Kasekese amesema mafunzo hayo aliyoyapata yatamsaidia kusimamia miradi ya maendeleo katika kijiji hicho itakayojitokeza japo kwa sasa miradi iliyopo niyamajengo ya Sekta ya Elimu.

Amesema baada ya Mafunzo haya atakwenda kuwaelimisha wananchi kijijini kuweza kusimamamia miradi yote pasitokee ubadilifu kwenye miradi itakayo letwa na serikali kwakuwa Mradi huo ameupokea vizuri bila mashaka yeyote baada ya kupatiwa mafunzo hayo atafanya kazi vizuri.

Kwa upande wake Halima Kitumba Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika amesema  kuwa Mradi huo utakwenda kusimamia na kuwaelekeza wananchi  baadhi ya Mambo yaliyoibuliwa na Ripoti CAG kwa mwaka 2017 Upande wa Elimu.

 Amesema washiriki hawa wameelekezwa kushiriki katika kuyapunguza au kuziondoa kabisa Maazimio ambayo yaliibuliwa na CAG kwenye Ripoti yam waka 2017 kwenye Elimu.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages