JUMUIYA YA WAZAZI CCM WAPANDA MITI 300


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Katavi Beda Katani (katikati)akipanda mti aina ya mwembe katika hosptali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo wakati alipotembelea hosptali hiyo kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo kuelekea maadhimisho ya miaka 44 ya kuzaliwa chama hicho.

 Na Mwandishi Wetu KTPC,Katavi.

Umoja wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wamefanikiwa kupanda miti mia tatu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo kwa ajili ya kujenga ustawi wa mazingira na kutunza uoto wa asili.

Upandaji wa miti huo umefanywa kuelekea maadhimisho ya kufikisha miaka 44 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM)  ambapo kuelekea kilele hicho,Jumuiya hiyo  imeamua kupanda miti.

Kaimu Katibu wa Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi,Hassan Tindo akizindua jana zoezi la upandaji miti katika viwanja vya Hosptali Teuli ya Rufaa ya Mkoa huo na kuongozwa na mgeni rasmi na mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Katavi Beda Katavi amesema kuwa kama wazazi wanawajibu kutunza mazingira ili yawe rafiki kwa watu.

Kamishina wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi,ACP Benjamin Kuzaga akipanda mti aina ya mwembe katika hosptali ya Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.


Tindo amesema wamefanikiwa kupanda miti katika Hosptali ya rufaa ya Mkoa wa Katavi,Viwanja vya shule ya msingi Mapinduzi ambapo zitajengwa nyumba za watumishi wa Chama,Hosptali ya Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo na Tanganyika,Ofisi Kuu ya CCM Mkoa  pamoja na shule ya Sekondari Milala iliyopo Manispaa  ya Mpanda.

‘’…tumepanda miti hii katika maeneo yote haya ni sehemu ya utekelezaji wa maagizo kutoka makao makuu ya chama cha mapinduzi tunapoelekea maadhimisho ya kufikisha miaka 44 ya chama chetu pamoja na kupanda miti hii pia tumeweza kugawa miti zaidi ya 100 kwa wananchi wa mkoa wetu’’ alisema Tindo.

Beda Katani ambaye ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) mkoa wa Katavi wakati wa upandaji wa miti amesema kuwa wananchi wanawajibu wa kupanda miti kwani maisha ya mwanadamu yanategemea miti kwa kuwa miti ni uhai.

Katibu wa Chama Cha Waadishi wa Habari Mkoa wa Katavi (KTPC),Paschal Katona (kulia)akipanda mti aina ya mwembe katika hosptali ya Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti huyo amesema kuelekea maadhimisho ya miaka 44 ya kuzaliwa CCM,Kama mkoa wamefanya juhudi kubwa kuwahaudumia wananchi kwa nguvu zote kwani kwa kufanya hivyo wamefanikiwa kupata matunda ya wananchi kukiamini chama hicho sambamba na kukichangua  chama bila kupingwa kwenye changuzi za serikali za mitaa pamoja na uchanguzi Mkuu kwa kuchaguliwa wabunge wote kutoka CCM pamoja na madiwani wa Kata zote.

Beda amesema kuwa kama mwenyekiti wa chama hicho anawajibu wa kuwatetea wananchi walio kichangua chama kukaa madarakani  na wala hana adhima ya kupinga kila jambo la serikali ili mradi tu kama jambo jema na linamasirahi kwa umma yuko tayari kulipongeza.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashaauri ya Wilaya ya Nsimbo Mohammed Rammadhani (kwanza kulia) akitoa maelezo ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa hospatali ya wilaya hiyo mbele ya mwenyekiti wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Katavi Beda Katani (pili kulia) wakati alipotembelea hosptali hiyo kuelekea maadhimisho ya miaka 44 ya kuzaliwa kwa chama.


Alifafanua kuwa kuelekea miaka 44 CCM,kama chama wanawajibu wa kuisimamia serikali katika utekelezaji wa ilani ya chama ambayo ni mkataba kati yao na wananchi.

Aidha amejivunia mafanikio makubwa yaliyofanywa na CCM katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kitaifa kama vile ujenzi wa reli wa gari moshi ya umeme,ujenzi wa miundombinu ya barabara kwa kiwango cha lami,imalishaji wa shirika la ndege nchini,uimarishaji wa upatikanaji wa huduma ya umeme vijijini na kuimarika kwa uchumi wa nchi kufikia wa ngazi ya kati.



Marry Anthony Mkazi wa Kijiji cha Milala Manispaa ya Mpanda ambaye ni mwanachama wa CCM,alipongeza viongozi wa chama kwa kuweza kufanya ziara hiyo ya upandaji miti pamoja na kukagua utekelezaji wa miradi.

Aliongeza kuwa kama wanachama wanajivunia kuona chama kina kuwa karibu zaidi na wananchi kwenye kuwatumikia kwa kuwa inaongeza hamasa  ya watu kuwa na imani kwa chama.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages