ASKOFU NZIGILWA AWAOMBA WANANCHI KUMWOMBA MUNGU TUPATE VIONGOZI WASIO BINAFSI.




Askofu wa Jimbo la Mpanda Mkoa wa Katavi Eusebius Nzigilwa akiongoza ibaada maalumu ya maombezi ya aliyekuwa rais wa Tazania Dkt John Magufuli aliyefariki hivi karibuni,Ibaada hiyo imefanya katika kanisa la mtakatifu Maria Immaculata Mpanda Mjini Mkoa wa Katavi na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali.
                            

Na  Walter Mguluchuma KTPC,Katavi 

Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda Askofu Eusebius  Nzigilwa amewaomba watanzania kuomba  Mungu   Nchi ipate viongozi watakao msaidia  Rais Samia  Suluhu Hassan ambao  hawata kuwa kwa manufaa yao binafsi  na waadilifu na wachapakazi ili  waweze kmsaidia kufanya kazi   Rais Samia   Suhulu  Hassan.



Waumini wa Kanisa la Roman Catholic waliohudhuria katika ibaada ya kumuombea aliyekuwa rais wa Tanzania Dkt John Maguli aliyefariki hivi karibuni.Ibaada hiyo imefanyika mjini Mpanda Mkoa wa Katavi,.
Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Mpanda Askofu Eusebius  Nzigilwa amewaomba watanzania kuomba  Mungu   Nchi ipate viongozi watakao msaidia  Rais Samia  Suluhu Hassan ambao  hawata kuwa kwa manufaa yao binafsi  na waadilifu na wachapakazi ili  waweze kmsaidia kufanya kazi   Rais Samia   Suhulu  Hassan.

Wito huu ameutowa  wakati wa ibada ya kumwombea  aliyekuwa Rais wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania Dkt John Magufuli iliyofanyika kwenye   Parokia Kuu ya Kanisa   Katoliki Jimbo la Mpanda  parokia ya Maria Imakulata  iliyohudhuriwa na  Mapadri wa Jimbo lote la Mpanda na viongozi wa Serikali wa Mkoa wa Katavi waliongozwa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Katavi ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph.

Nzigilwa ameeleza kwenye  mahubiri yake kuwa  wapo baadhi ya watu huwa wanataka kuwa viongozi ili waongoze kwa manufaa yao binafsi.



Kanisa la Jimbo Kuu Mpanda la Mtakatifu Maria Immaculata Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi.
Hivyo amewataka watanzania wamuombe  Mungu Nchi hii ipate viongozi ambao hawatakuwa kwamanufaa yao binafsi na wawe waadilifu, wazalendo , wachapakazi na wanao mcha Mungu kama alivyokuwa  hayati Rais  John Magufuli ili waweze kumsaidia Rais Samia     Sluu Hassan.

Amesema Taifa  baada  ya kupitia kwenye changamoto  hii watanzania wanaamini kuwa   Taifa litaendelea kusimama kama lilivyokuwa .

Askofu  Nzingilwa alieleza kuwa yeye  kabla ya Rais  Magufuli haja fariki  Dunia wakati alipokuwa amelazwa  Hospitalini alikuwa akiwasiliana na wasaidizi wa  karibu  wa hayati Magufuli kwani alikuwa akifahamiana nao .

Na  katika mwasiliano yake na wasaidizi hao walimwambia kuwa hayati Magufuli  wakati akiwa kitandani alipenda sana kuimba nyimbo za Dini za Kanisa la RC na alikuwa akiwashirikisha na wasaidizi wake kuimba nyimbo hizo .

Pia wamemweleza kuwa alikuwa akipenda sana muda wote kutembea na rozali  akiwa ameiweka kwenye mfuko wake wa saruali na alikuwa haiachi hata siku moja na aliitumia zaidi kusali hasa pale ambapo alipokuwa na jambo linamtatiza .

Amesema siku moja kabla ya kifo chake aliwaomba wasaidizi wake wamwite  KadrinaliPolikapo  Pengo na Paroko wa  Paroka ya Mtakatifu Peter  Ositabeyi.



Askofu wa jimbo la Catholic Jimba la Mpanda Mkoa wa Katavi Eusebius Nzigilwa(nne kushoto)akiwa na Mkuu wa wilaya ya Mpanda,Bi Jamila Yusuph (tatu kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja na mapadri na viongozi wa serikali baada ya ibaada ya kumwombea aliyekuwa rais wa Tazania Dkt John Magufuli aliyefariki hivi karibuni.
Ameeleza kuwa Kadrinali  Pengo  na Paroko  wa parokia hiyo waliweza kufika Hospitalini hapo na waliweza kuongea nae hayati Magufuli na siku iliyofuata alifariki Dunia .

Hari hiyo inaonyesha kuwa   hayati Magufuli amekuwa  katika imani na ndio maana aliongea na viongozi wa Dini kwa mara ya mwisho.

Amewaomba Wanzania kumwombea  Rais Samia Sluu  Hassan  katika  kipindi hiki cha majonzi aweze kupata Makamu  wa  Rais atakaeweza kumsaidia kufanya kazi .

Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa   wa Katavi ambae ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila  Yusuph alisema  hakuna haja ya kuendelea  kufadhaika na badala yake tuendelee kumwezi kwa kufanya kazi .

Amesema katika kipindi chake cha uongozi amefanya mambo makubwa kwa Mkoa wa Katavi kama vile ujenzi wa barabara za kiwango cha lami zinazounganisha Mkoa huu na Mikoa mingine,  ujenzi wa vituo vya afya nane  Hospiitali  za Wilaya tatu na moja ya Rufaa ya Mkoa ,ujenzi wa bandari ya Karema, safari za ndege,ujenzi wa reli ya standa geji na miradi  ya maji .

Monsinyori Padri  George Kisapa ambae ni  makamu wa Jimbo Katoliki la Mpanda alisema kuwa toka amekuwa  Padri haja wahi kuona maendeleo yaliopatikana katika Mkoa wa Katavi na nchi kwa kipindi kifupi kama alivyofanya Rais Magufuli.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages