TAKUKURU KATAVI  WAMKAMATA  KATIBU WA KITONGOJI KWA RUSHWA .




Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi,Christopher Nakua

Na  Walter  Mguluchuma Katavi 

Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Takukuru Mkoa wa Katavi  wamemkamata  katibu wa Kitongoji  cha Magula     Tarafa ya  Nsimbo  Wilaya ya  Mpanda  Egid  Damas Ntila  maarufu  kwa jina la  mwalimu  Egid  Peter kwa kosa  la kuomba  rushwa  ya shilingi laki  tatu   kinyume  na kifungu cha  15 cha sheria  ya kuzuia  na kupambana na Rushwa  Namba 11 ya mwaka 2007.


Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa Takukuru Mkoa wa Katavi  wamemkamata  katibu wa Kitongoji  cha Magula     Tarafa ya  Nsimbo  Wilaya ya  Mpanda  Egid  Damas Ntila  maarufu  kwa jina la  mwalimu  Egid  Peter kwa kosa  la kuomba  rushwa  ya shilingi laki  tatu   kinyume  na kifungu cha  15 cha sheria  ya kuzuia  na kupambana na Rushwa  Namba 11 ya mwaka 2007. 

Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi  Cristopher  Nakua aliwaambia wandishi wa  Habari wa vyombo mbalimbali kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na Takukuru  hapo  machi  11 huko katika kitongoji cha Magula Kata ya Sitalike.

Katika tukio hilo  mtuhumiwa  Egid  Ntila   ambae ni  Kaimu   Katibu  Katibu  wa Serikali  ya Kitongoji  cha  Magula  kilichopo   katika  Kijiji cha  Mtisi  Kata ya  Sitalike  Wilaya ya Mpanda  alipokea Rushwa ya  fedha kiasi cha shilingi elfu  Hamsini  ikiwa ni sehemu  ya shilingi laki tatu  ambazo alikuwa ameziomba kutoka kwa mlalamikaji  jina limehifadhiwa .

 Nakua ameeleza kuwa  mtuhumiwa huyo aliomba Rushwa hiyo    ya fedha  ili amuuzie  mlalamikaji  eneo  la kufanyia biashara  katika soko  jipya lililoko kwenye kitongoji hicho ambapo viwanja vilikuwa vikitolewa   kwa ajiri ya watu kufanyia biashara hapo .

Amesema kuwa utaratibu wa kutowa viwanja vya kufanyiia biashara hapo vilikuwa vikitolewa bure  kwa wale ambao walikuwa wamewahi  kuomba hata hivyo Katibu huyo hakufanya hivyo na badala yake alimtaka  mlalamikaji ampatie kasi cha  shilingi laki tatu  kama rushwa ndio aweze kumpatia eneo kwenye soko hilo

  Amesema  baada ya  mtuhumiwa kuomba  Rushwa hiyo kutoka kwa mlalamikaji  Takukuru walipata taarifa hizo na ndipo walipo andaa mtego na kufanikiwa kumkamata mtuhimiwa huyo  akipokea kiasi cha Tshs 50 000 katia ya shilingi laki tatu .

 Takukuru Mkoa wa Katavi wanaendelea na uchunguzi  wa tuhuma zinazomkabili  huyo  na pindi utakapokuwa  umekamilika  na kuthibitika  mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani ili akajibu tuhuma zinazo mkabili .

 Katika  hatua nyingine  Takukuru  Mkoa wa Katavi  kwa kushirikiana na ofisi ya  Taifa  ya Mashitaka  Mkoani Katavi  imefanikiwa  kufungua kesi mbili  Mahakamani  za makosa ya Rushwa .

 Nakua alizitaja kesi hizo ni  kesi ya kwa inawahusu   Pridance  Anacredo  pamoja na  Varanto  Wiliamu  ambao walikuwa ni viongozi  wa  Amcos  Mishamo

Amesema  watu hao  wameshitakiwa kwa tuhuma za  kufanya kosa la kutumia matumiz yai madaraka  yao vibaya  kinyume  na kifungu  cha 31 cha sheria ya kuzuia na kupambana na Rushwa  Na 11 ya mwaka  2007  wameshitakiwa  kwa huhuma za  kujipatia  jumla  ya shilingi milioni nne  kama mkopo   isivyo  halali  na kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mpanda .

Kesi ya pili ameitaja kuwa   ni inayomkabili  Juma  Mnyongalule  ambayo imefunguliwa katika Mahakama  ya Hakimu  Mkazi  wa Mkoa wa  Katavi  ambapo mtuhumiwa  ameshitakiwa  kwa kujipatia kiasi cha Tshs 3,750,000 isivyo halali.

Amesema mtuhumiwa huyo  aliendelea kulipwa  na kupokea fedha  za mshahara  kutoka  Shirika la Reli  Tanzania alikokuwa akifanyia kazi  kama fundi  Mchundo  maarufu  Pigilia  wakati huo akiwa  sio mwajiriwa  tena wa  shirika  la Reli  Tanzania kwa mujibu wa sheria

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages