Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi, Salehe Mbwana Mhando amemtaka Mhandisi anayesimamia ujenzi wa Kituo cha Afya cha Kata ya Mnyagala kukamilisha ujenzi wa kituo hicho ili kianze kuwahudumia wananchi.

Agizo hilo ametoa mkuu wa wilaya hiyo kuwa ifikapo mwaka huu April 30 kiwetayari na kuanza kutumika kwa ajili ya kuondoa adha kwa wananchi ambao mpaka sasa hawana duduma za Afya Katika Kata hiyo.

Mhando ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake akikagua miradi mbalimbali ya Afya na barabara ambapo meelekeza mradi huo ukamilike mapema mwezi huu.
Diwani wa Viti Maalum Kata ya Mnyagala Mhe Amina Lumbwe anaomba baadhi ya huduma kama kliniki ya Watoto zimekwisha kuanza kutolewa.

Ibrahimu Bashiru ni Msanifu Majengo katika Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi ambae anabainisha Kuwa Mradi wa Kituo cha Afya Mnyagala umefikia asilimia 98 ya ujenzi.
