Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda.
Na Walter Mguluchuma KTPC,Katavi

Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda amewaomba watanzania waendelee kumwomba Mungu kwa kuwavusha salama katika kipindi kigumu ambacho kilikuwa akija wahi kutokea hapa Nchini cha kuondokewa na Rais ambae alikuwa bado yupo madarakani akiwa haja maliza muda wake wa uongozi
Pinda alitowa ombihilo kwa Wanzania wakati alipokuwa akiwahubia waumini wa Kanisa katoliki kwenye Kanisa Kuu la Jimbo la Mpanda Parokia ya Maria Imakulata wakati wa ibada ya juma pili kwenye ibada ya misa ya pili iliyoongozwa na Padri Filbert Baligwa ambae pia ni mwasibu wa Jimbo la Mpanda .
Alisema Wanzania waendelee kumwomba Mungu kwa kuwawezesha kuvuka salama katika kipindi kigumu cha kuondokewa kwa ( kifo )cha aliyekuwa Rais wa Tanzania John Magufuli wakati akiwa bado madarakani .
Amebainisha kuwa ilikuwa haija wahi kutokea katika nchi hii kuondokewa na Rais ambae bado alikuwa kwenye kipindi cha uongozi tulikuwa tunaondokewa na Marais waliyo maliza muda wao ``Alisema Pinda
Alisema kuwa tuendelee kumwombea kwa Mungu kwani wakati wa maisha yake hayati Magufuli alikuwa na hofu ya Mungu na ndio maana kila mara alikuwa na hofu ya Mungu .
Pinda alieleza kuwa ni jambo la kushukuru kwa Nchi ya Tanzania kumpata Rais Mama Samia Hassn Suluhu ambae walikuwa wakipanga mipango pamoja na Hayati Magufuli .
Yeye anaamini kuwa yale yote yalikuwa yamepangwa kufanyika kwenye nchi hii wakati wa uongozi wa hayati Magufuli yataendelea kutekelezwa pasipo shaka yeyote
Hivyo ni vema Wanzania wakampa ushirikiano mkubwa Rais Samia Hassn Suluhu ambae ameanza vizuri kuongoza nchi yetu.
Alisema kuwa wapo baadhi ya watu walikuwa na mashaka na kuongozwa na Rais mwanamke lakini mama huyo ameisha waondolea mashaka hayo na ndio maana mara kwa mara amekuwa akisema kuwa anaweza na kweli amaweza`` alisema Mizengo Pinda
Kwa upande wake Padri Filibert Baligwa aliwaomba Watanzania wawaombee viongozi wa sasa walioko madarakani ili waweze kuongoza nchi kwa upendo na amani ili tuweze kupata manufaa ya nchi kwa wakati huu na wakati ujao

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Katavi,Beda Katani.