
Diwani wa Kata ya Shanwe Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi,Hafidhi Masumbuko akizungumza na wananchi wa kata hiyo namna ya kutekeleza ujenzi wa miradi ya maendeleo.
Na Alex Ngereza KTPC,Mpanda. Diwani wa Kata ya Shanwe Manispaa ya Mpanda
Mkoa wa Katavi,Hafidhi Masumbuko amesema kuwa atahakikisha ujenzi wa kivuko
kinachounganisha Kata mbili za Misukumilo na Kilima hewa kuwa zinajengwa haraka
ili kurahisisha shughuri za maendeleo. ![]() Diwani huyo amesema hayo leo wakati anazungumza na wananchi wa kata ya Shanwe namna ambavyo amejidhatiti kupitia baraza la madiwani anakwenda na ajenda kuomba serikali kutenga fedha za ujenzi wa kivuko. ![]() Ameleza kuwa kama kivuko hicho kitajengwa kwa
wakati kitakuwa chachu ya maendeleo kwenye kata zote hizo pamoja na manispaa ya
Mpanda hasa kwenye Nyanja ya kibiashara
ambapo watu watatumia kusafirishia mizingo. “ nitakwenda kuhakikisha na jenga hoja ya
kufanikisha hili kwa sababu kimekuwa kilio cha watu cha muda mrefu sana”
amesema diwani huyo. Katika hatua nyingine Diwani huyo amewashukia vikali walio tafuna fedha za ujenzi wa Zahati ziliozochangwa na wanachi kuzirudisha haraka kabla ya kuchukua hatua kali zan kisheria. ![]() “Ujenzi wa Daraja hilo utasidia kuepusha
madhira ambayo yamelipotiwa kwa mara kadhaa ya watoto kupoteza Maisha”
amesisitiza Diwani. Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara baadhi
ya wananchi wamesema kuwa mara kadhaa kumekuwa na matukio mengi ya watoto
kusombwa na maji kwenye mto wa kata ya Shanwe pamoja na Misukumilo. Daniel Katigili amempogeza diwani kwa kuonesha juhudi za kuwasaidia wananchi kuondokana na kero hiyo ya muda mrefu huku akimwahidi kumuuga mkono kwa kila jambo ambalo atakuwa na nia ya kulifanya kwenye kata hiyo. ![]() “nafikiri mimi wamepita madiwani wawili kabla
yako nimewaona nikiwa hapa sijapata diwani mwenye maneno ya kuwafariji wakazi
wake kama wewe Mh Diwani wa sasa …nafikiri Mungu atakusaidia. Aidha Daniel alieza baadhi ya kero ambazo wanakabiliwa nazo kama wazee hasa kwenye ubovu wa miundomibu ya barabara,hivyo ukiwa mzee njia nzima utakuwa ni mtu wa kuaguka anguka. ![]() Said Hassain amesema kuwa kwenye sekta ya
michenzo na burudani anapaswa kuiangalia kwa makini maana ni sekta ya ambayo inauwezo
wa kuajili vijana wengi. Amesema licha ya kuajili vijana wengi
inapaswa kutengenezewa mazingira mazuri ya vijana kutumia fursa hiyo vizuri. |