JIUXING TANZANIA MINING YA SAIDIA JAMII NSIMBO

Afisa uhusiano wa Kampuni ya uchimbaji wa Mdaini ya Jiuxing Tanzania Mining company limited Anselm Mjinga Kulia akitoa taarifa ya utendaji kazi wa Mgodi huo kwa mkuu wa mkoa wa katavi Mwanamvua Mrindoko alipotembelea Mgodi huo. 

Na Paul Mathias 

Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Jiuxing Tanzania Mining Company Limited inayofanya kazi zake katika Vijiji vya Ibindi na Mtakuja Hlmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi imesema kuwa Tangu waanze kazi mwezi novemba Mwka jana 2022 wamesaidia jamiii katika Nyanja za Elimu,Usalama,na Miundombinu.

Mhandisi Andrew Mwalugaja Meneja wa Madini Mkoa wa Katavi akitoa maelezo kwa mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko juu ya uwepo wa Kampuni ya Jiuxing Tanzania company limited katika Kijiji cha Ibindi halmashauri ya Nsimbo mkoa wa katavi. 
Kampuni ya uchimbaji wa madini ya Jiuxing Tanzania Mining Company Limited inayofanya kazi zake katika Vijiji vya Ibindi na Mtakuja Hlmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi imesema kuwa Tangu waanze kazi mwezi novemba Mwka jana 2022 wamesaidia jamiii katika Nyanja za Elimu,Usalama,na Miundombinu

Hayo yamebainishwa na Afisa uhusiano wa Mgodi huo Anselm Mjinga wakati akitoa taarifa ya utendaji wa Mgodi kwa mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko alipotembelea Mgodi huo ili kujionea namana unavyofanya kazi zake.

Anselm amesema kuwa wamewkuwa lafiki na jamii inayo wazaunguka kwa kuendelea kuwa na mahusaiano mema na jamii kwa kuweza kusaidia jamii katika Nyanja za elimu na ulinzi kwa kusaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi katika kijiji cha Ibindi na hapa anasema

“hatuja fikia kwenye uzalishaji lakini kuna mafanikio mfano kwenye ujirani mwema hii Kampuni ipo vizuri sana na viongozi wa serikali kwa ujumla kwa kusapoti ujenzi wa kituo cha polisi Ibindi kwa kutoa Tofali 40000 za Block zenye thamani ya shilingi Milioni 5 hivyo mkuu wa mkoa tuna mahusiano mazuri na jamii amsema ‘’Anselm

Pamoja na hayo amebainisha kuwa katika sekta ya elimu wamekuwa wakisaidia katika suala zima la Mdawati kwa shule zinazopatikana katika Kwenye maeneo wanayofanyia kazi kwa lengo la kutambua umuhimu wa elimu katika jamii hizo na Taifa kwa Ujumla.

“tumesapoti Madawati kwa shule ya Sekondari Ibindi na Sekondari ya Kapalala kama ujirani Mwema tumetoa Madawati 60, Ibindi tumepeleka madawati 30 na Kapalala tumepeleka Madawati 30”

Kuhusu ajira kwa vijana katika Mgodi huo amesema hadi sasa wameweza Kuajiri  watu 20 ambao wapo kwenye Mkataba na wanatalajia kuajili wafanya kazi 500 huku kipaombele kikiwa kuajiri vijana kutoka vijiji vinavyozungukwa na Mgodi huo pamoja na vijana kutoka halmashauri ya Nsimbo kwa kusaidia jamii kwenye suala la Ajira.

Katika hatua anyingine amsema kuwa kunachangamoto katika Mgodi wa Mtakuja ambapo kuna maeneo ya Ekari Mbili ambazo wamiliki wake wanadai fidia ya kulipwa hivyo kuwapachangamoto katika kufanya shughuli hiyo.

,,tunachangamoto moja kwenye Mgodi wa Mtakuja kuna Ekari mbili za wamiliki wawili wale watu tulitamani tumekaa nao mezani angalau waweze kutuachia hayo maeneo hata kwa kuwalipa fidia au kuwabadilishia maeneo mengine ili tuweze kuendelea na shughuli za uzalishaji pale kuna mitambo tayari imefika pale tulitamani tuweze kuijenga pale tunaobwa fidia ya hadi Milioni 600 hii inatupa changamoto Mh Mkuu wa Mkoa tungeobwa kuasaidiwa katika hilo ili tuendelee na kazi amesema Anselm.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewakalibisha kampuni hiyo katika mkoa wa Katavi na kuchangamkia fursa ya uwekezaji katika sekta ya madini kwa kutambua umuhimu wa wawekezaji.

Mkuu wa mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wa kwanza [kushoto] akiwa katika mgodi wa Jiuxing Tanzania Companya Limited alipotembelea Mgodi huo
 
“hongereni sana kwa kuiona Fursa na kulizika na mazingira ya Katavi na mkaamua kuja kuwekeza hapa kwa Gharama kubwa nataka niwahakikishie kwamba kama vile ambavyo Mh Rais amelenga kuweka mazingira bora kwa wawekezaji mbalimbali kwenye sekta zote tutawapa ushirikiano na tutaendelea kuboresha miundombinu ili wawekezaji waweze kufanya shughuli zao katika mazingira mazuri “amesema Mrindoko.

Kuhusu changamoto ya Mgogoro baina ya wamiliki wa ekari Mbili katika kijiji cha Mtakuja mkuu huyo wa mkoa wa Katavi amemwelekeza mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nsimbo kuona namna ya kulitatua kwakuwa kawakuwa tayari limeshalipotiwa kwake.

“Kuhusu lile la mgogoro nimtake mkurugenzi ambae alililipokea amabae lipo kwake alimalize kwa taratibu zilizopo na kama itaonekana kwamba kuna matatizo zaidi mkuu wa wilaya pia yupo na mawakilishi wake yupo hapa naamini kuptia ofisi hizi mbili kwa kushirikiana na meneja wa madini Mkoa naamini tatizo hilo litakwisha vizuri”

Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa serikali katika mkoa wa Katavi inaendelea kuwakalibisha wawekezaji kwa lengo la kusisimua uchumi wa mkoa wa Katavi kwa ujumla.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages