ML 500 ZATOLEWA KUJENGA HOSPITALI YA WILAYA MBINGA


Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma,Desdelius Haule kushoto na Mgurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo,Juma Mnwele kulia wakichimba kisiki katika eneo la mradi wa ujenzi wa Hospitali ya halmashauri inayojengwa kijiji cha Kigonsera.

Na Muhidin Amri KTPC,Mbinga.

SERIKALI imeipatia Halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvuma kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga Hospitali  ya Wilaya ikiwa ni  mkakati wa kuimarisha na kuboresha  huduma za Afya hapa nchini.


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri wilaya ya Mbinga  Juma Mnwele alisema, tayari wamepokea fedha hizo kutoka Serikali Kuu  na wameshaanza kujenga  Hospitali  hiyo katika kijiji cha Kigonsera kata ya Kigonsera.


Mnwele amesema,  ujenzi wa Hospitali hiyo utafanyika kwa awamu kulingana na fedha zitakazoletwa na Serikali na kwa kuanzia wataanza kujenga majengo ya  vipaumbele kama jengo la wagonjwa wa nje(OPD) na maabara na kichomea taka na majengo mengine yataendelea kujengwa kulingana mapato.


Amesema, kwa kazi zilizofanywa na wananchi wa Kigonsera kusafisha eneo  zimesaidia kuokoa fedha nyingi ambazo zitasaidia kuongeza majengo mengine ya kutolea huduma na kuwaomba wananchi hao kuendelea kufanya kazi za kujitolea katika mradi huo.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinda Desdelius Haule, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kutao fedha  kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo na miradi mingine ya maendeleo inayokwenda kuharakisha  kukua kwa uchumi.


Amesema, ujenzi wa Hospitali hiyo ni matokeo mazuri ya utendaji wa Serikali ya Chama cha Mapinduzi ikiwa ni sehemu ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama hicho kuimarisha na kuboresha huduma za Afya kwa wananchi.


Katika kuunga mkono juhudi za Serikali Kuu,SerikaliI ya kijiji cha Kigonsera,imetoa zaidi ya ekari 35  za ardhi ili  kujenga Hospitali hiyo.

Mwenyekiti wa kijiji  hicho Emanuel Ngongi amesema, kwa kutambua changamoto walizokabiliana nazo kwa muda mrefu serikali ya kijiji kupitia mkutano Mkuu wa kijiji  uliowajumuisha wananchi wote umeridhia kutoa ardhi iliyotengwa  baada ya Halmashauri  ya wilaya kuwa na wazo la kujenga Hospitali.


Ngongi amesema, wameamua kutoa ardhi hiyo bure ili kutekeleza mradi huo ambao unakwenda kumaliza changamoto ya huduma za afya  kwa wakazi wa kijiji hicho ambao sasa wanalazimika  kwenda hadi Hospitali ya Misheni Peramiho na  Hospitali ya Rufaa Songea mjini umbali wa km 100  

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages