Na Walter Mguluchuma KTPC,Katavi.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Ummy Mwalimu amepiga marufuku huhamishwa kwa walimu na Watumishi wa Afya wanao fanya kazi katika Mikoa ya Katavi , Kigoma , Kagera. Lind na Mtwara mpaka hapo kuwe na watumishi wa kutoka sehemu nyingine ambao watakao chuo nafasi zao.Maagizo hayo ameyatowa kwa nyakati tofauti wakati alipokuwa akiongea na wananchi wa Halmashauri ya Tanganyika, na Halmashauri ya Nsimbo kwenye Vijiji vya Ugala Halmashauri ya Nsimbo na Halmashauri ya Tanganyika .
Alisema kuwa Mikoa hiyo ilikuwa na idadi ya watumishi wachache wa idara hizo mbili lakini Serikali kwa sasa imeelekeza nguvu kwenye Mikoa hiyo ili kupunguza tatizo hilo ambalo limekuwa likiikabili Mikoa hiyo ambayo mazingira yake yameimalika
Alimwangiza katibu Mkuu wa Tamisemi kuhakikisha kuwa walimu na watumishi wa Afya wanao fanya kazi kwenye Mikoa ya Katavi , Kigoma , Lindi na Mtwara kutohamishwa mpaka hapo watakapokuwa wamewahamishia watumishi wengine kushika nafasi zao .
Alisisitiza kuwa endapo kuna mwalimu au mtumishi wa afya anae fanya kazi kwenye mikoa hiyo ataondolewa pasipo kupeleka kwanza mtumishi mwingine wa kuchukua nafasi yake atakuwa mkali kwa mtu atakae kuwa ameidhinisha uhamisho huo .
Kuhusu wa Kurugenzi watendaji wa Halmashauri ambao watateuliwa hivi karibuni kwenye mkeka ambao utakao toka watambuekuwa watakuwa wanapimwa kwa jinsi ambavyo walivyofanya kazi ya kutekeleza miradi ya maendeleo kutokana na fedha asilimia 40 ya mapato yao ya ndani .
Waziri Ummy alibainisha kuwa Wakurugenzi hao watakuwa wanapimwa kila baada ya miezi mitatu kwa jinsi walivyo kufanya mapato yao ya ndani na jinsi walivyotumia fedha hizo kwa ajiri ya kufanyia shughuli za miradi ya maendeleo kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha fedha zinazokusanywa kwenye Halmashauri za mapato yao ya ndani zinatumika kwa ajiri ya kutatua kero za wananchi kwenye Halmashauri zao.
Waziri Ummy alibainisha kuwa Wakurugenzi hao watakuwa wanapimwa kila baada ya miezi mitatu kwa jinsi walivyo kufanya mapato yao ya ndani na jinsi walivyotumia fedha hizo kwa ajiri ya kufanyia shughuli za miradi ya maendeleo kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha fedha zinazokusanywa kwenye Halmashauri za mapato yao ya ndani zinatumika kwa ajiri ya kutatua kero za wananchi kwenye Halmashauri zao.
Alifafanua kuwa Tamisemi wanampango wa kuangalia upya mgao wa fedha za barabara ili waweze kuzitowa kulingana na ukubwa wa Halmashauri kwani mgao walikuwa wamepanga wa kutowa milioni 500 kwa kila haukuzingatia ukubwa wa maeneo hivyo mgao huo mpya utazingatia ukubwa wa Jimbo husika .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko alisema kuwa Mkoa wa Katavi unaupungufu wa watumishi wa karibu kwenye sekta zote zilizopo kwenye Mkoa huu.
A lisema licha ya kuwa na upungufu wa watumishi kazi zimekuwa zikifanywa na watumishi hao ambao walioko kwenye Mkoa wa Katavi kama kawaida ambapo kwenye baadhi ya idara mtumishi mmoja amekuwa akifanya kazi ambazo zinazotakiwa kufanywa na watumishi wawili .
Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe alimshukuru Waziri wa Tamisemi kwa kuwahaidi wananchi wa Kata ya Ugala kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajiri ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya ugala kitakacho saidia kuondoa vifo vya mama na mtoto.
Alieleza wananchi wa kata hiyo walikuwa wakilazimika kutembea umbali wa kilometa 76 kwenda kufuta huduma ya upasuaji kwenye hospital ya Wilaya pindi mjamzito anapokuwa ameshindwa kujifungua hali ambayo imekuwa ikisababisha wajifungulia njiani na wengine kupoteza maisha .
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko alisema kuwa Mkoa wa Katavi unaupungufu wa watumishi wa karibu kwenye sekta zote zilizopo kwenye Mkoa huu.
A lisema licha ya kuwa na upungufu wa watumishi kazi zimekuwa zikifanywa na watumishi hao ambao walioko kwenye Mkoa wa Katavi kama kawaida ambapo kwenye baadhi ya idara mtumishi mmoja amekuwa akifanya kazi ambazo zinazotakiwa kufanywa na watumishi wawili .
Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Anna Lupembe alimshukuru Waziri wa Tamisemi kwa kuwahaidi wananchi wa Kata ya Ugala kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajiri ya kuanza ujenzi wa kituo cha afya ugala kitakacho saidia kuondoa vifo vya mama na mtoto.
Alieleza wananchi wa kata hiyo walikuwa wakilazimika kutembea umbali wa kilometa 76 kwenda kufuta huduma ya upasuaji kwenye hospital ya Wilaya pindi mjamzito anapokuwa ameshindwa kujifungua hali ambayo imekuwa ikisababisha wajifungulia njiani na wengine kupoteza maisha .



