MANISPAA YA MPANDA INA CHANGAMOTO YA WANANCHI KUJITOLEA.

Na Walter Mguluchuma-KTPC,Katavi .
Manispaa ya Mpanda  katika Mkoa wa  Katavi inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa walimu zaidi ya 700 wa Shule za msingi na wananchi kuwa na mwitikio mdogo wa kufanya shughuli za Maendeleo hari ambayo imekuwa ikisababisha miradi kutokamilika kwa asilimia mia moja.

 Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda  Michael  Nzyungu wakati wa kikao cha mwisho wa mwaka cha Baraza la Madiwani wa Manispaa ya Mpanda kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo .

Amesema kuwa    katika  Halmashauri hiyo kuna upungufu wa walimu wa shule za msingi karibu katika shule zote zilizopo katika  katika Manispaa ya  Mpanda hali ambayo imekuwa ikiwafanya walimu kufanya kazi kubwa ya ufundishaji .

 Idadi ya walimu ambao wamepungua ni walimu  767 kwenye   Halmashauri hiyo ambayo ni idadi kubwa hivyo wanaiomba Serikali iendelee kuwapatia walimu ili kuweza kuondoa tatizo hilo la upungufu wa walimu .

  Aidha  Manispaa ya  Mpanda inakabiliwa na tatizo la kutokamilika kwa miradi  ya maendeleo kutokana na wananchi kuwa na mwitikio mdogo wa kuchangia shughuli za Maendeleo na kufanya miradi kutokamilika kwa asilimia mia moja .

 Nzyungu alifafanua kuwa serikal imeisha towa maelekezo ya kujenga maboma ya shule na  Zahanati na wakisha kamilisha ujenzi wa maboma Serikali hutowa fedha kwa ajiri ya kumalizia maboma yanayokuwa tayari kutokana na wananchi kutokuwa na mwitikio wa kuchangia kazi ya maendeleo Manispa wamekuwa wakilazimika kutumia fedha za mapato yao ya ndani kujengea maboma hayo  ambapo fedha hizo zingeweza kutumika kwenye shughuli nyingine  endapo kama wananchi wangejitolea.

 Meya wa Manispaa ya Mpanda  Haidari  Sumry aliwataka Madiwani  wahamasishe wananchi wao kwenye Kata wanako toka  ili wananchi hao waweze kushiriki katika kufana shughuli za kufanya kazi kwenye miradi ya maendeleo

Alisema kuwa mwaka huu Serikali imewaletea fedha nyingi  kwenye miradi ya maendeleo kuliko hata walivyoomba hivyo nii vema  madiwani  madiwani waendelee kushirikiana na kusimia miradi ya maendeleo na matokeo yake yatazidi kuonekana  zaidi .

  Meya  huyo wa Manispaa alieleza kuwa mwaka wa fedha uliopita wamejitahidi sana kukusanya fedha za mapato ya ndani na kuweza kuvuka zaidi ya asilimia mia moja  kwa hivyo kwa mwaka huu wazidi kukusanya zaidi mapato hayo na kuyasimia vizuri .

 Nae  Diwani wa Kata ya Mwamkulu  Alipi  Katani aliomba kuwe na utaratibu wa  maafisa kilimo kufika kwenye shule na kutowa elimu kwa wanafunzi ili wananchi wanao kuwa wanazunguka kwenye maeneo hayo ya shule waweze kujifunza utaalamu wa kilimo kwenye mashamba darasa ya kwenye shule hizo.

 


Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages