POLISI KWA KUSHIRIKIANA NA TANAPA WAKAMATA SILAHA YA KIVITA NA MENO YA TEMBO.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi Benjamin Kuzaga akitoa taarifa kwa wanahabari mkoani humo ya kukamata majangili.

Na Walter Mguluchuma-KTPC,Katavi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na kikosi maalumu   cha kupambana na ujangili na uhalifu na Askari wa TANAPA  wamefanikiwa kukamata meno ya tembo yenye  uzito wa kilogramu  4.72 na silaha kali ya kivita aina ya AK 47  ikiwa na  magazini  moja  yenye risasi 28 na nyama ya wanyama pori yenye uzito wa zaidi ya kilo 30.

 Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Benjamin aliwaambia wandishi wa  Habari  kuwa katika msako huo waliofanya  katika maeneo mbalimbali ya Mkoa  kukabiliana na uhalifu na ujangili  katika msako huu waliweza kukamata watuhumiwa tisa  .

Katika tukio la agosti 22 majira ya saa tatu usiku  huko  katika maeneo ya mji mwema  Kata ya Majengo Manispaa ya Mpanda  waliweza kumkamata  Hamza  Jonsia  akiwa na  nyara za Serikali  vipande viwili  vya meno ya tembo  yenye uzito  kiligramu 4.72 ambayo  thamani yake bado haija fahamika.

Mtuhumiwa huyo  alikamatwa baada ya kuwa ametiliwa mashaka  na baada ya kuwa  amepekuliwa  walimkuta akiwa  na vipande  hivyo vya meno ya tembo akiwa amehifadhi  ndani ya  begi  la rangi nyeusi  likiwa limeandikwa Bob marly

 Katika msako huu uliendelea hapo mnamo  Agost 23 majira ya saa nne usiku  huko katika  maeneo  ya  magogo  ndani ya  Hifadhi ya Taifa  ya Katavi  waliwakamata watuhumiwa nane wakiwa na bunduki ya kivita  aina ya  AK 47   yenye  namba  UC 1988  ikiwa na magazini moja na risasi 28.

Kamanda Kuzaga  alisema  pia watuhumiwa  hao  walikamatwa na  jino moja la tembo  lenye uzito wa kilogramu 20 za  nyama  ya  mnyama huyo na pia  walikamatwa na pikipiki  yenye Namba T 465AXL   aina ya SunLg  iliyokuwa imebeba nyama pori  aina ya ngiri yenye kilogramu 35.

Kamanda Kuzaga amewataja watuhumiwa hao nane kuwa ni  Fransis    Thadeo  Geremamano  mkazi wa Kigamboni Manispaa ya Mpanda , Leonald  Mtende  Ngoyani (48) Mkazi wa Kawajense Manispaa ya Mpanda , Gabriel Milambo (42) Mkazi wa Kawajens, Phibart Libuma (30)  mkazi wa Makazi ya wakimbizi Mishamo, Agustin Clavery Silasi (19) Mkazi za Sitalike na Peter Simon Matege (42) mkazi wa Shanwe.

Aidha Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi alitowa rai kwa wananci wanaojihusisha kufanya biashara haramu za magendo kama vile unaribifu wa rasilimali za taifa kwa kufanya vitendo vya ujangili uwindaji haramu kuacha na badala yake wajikite kufanya shughuli halali za kuwaingizia kipato.

Naye Afisa Mhifadhi anayesimamia kitengo cha himasheria na ulinzi wa kimkakati katika hifadhi ya Katavi (KANAPA), Lameck Matungwa alisema kuwa kama wahifadhi nchini wataendelea kufanya ushirikiano na wadau mbalimbali ili kutokomeza ujangili nchini.

Matungwa alibainisha kuwa kuendelea kuingizwa kwa siraha ndani ya hifadhi kunaleta madhara makubwa sio kwa tembo tu bali hata kwa wanyama wengi na kuathiri usitawi wa sekta ya utalii nchini ambapo imekuwa ikitegemea uwepo wa wanyama ambao huwa kivutio kikubwa kwao.

Vilevile alitoa wito kwa wananchi wanaozunguka hifadhi wasioneka kuwa ndio chanzo cha kuwakaribisha waharifu kwani miongoni mwa watu waliokamatwa na jeshi la polisi ni watu wanaoishi karibu na hifadhi.Hivyo wanapaswa kuwa sehumu ya watu wanaotoa taarifa mapema kwa polisi pindi wanapoona viashiria vya ujangili.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages