WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA KUANZA ZIARA YA SIKU TATU KATAVI

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko.


Na Walter Mguluchuma KTPC,Katavi.

Waziri  Mkuu  Kassm Majaliwa anatarajia kuanza ziara ya siku tatu Mkoani Katavi ya kukagua miradi mbalimbali ya Maendeleo inayoendelea kutekelezwa Mkoani hapa ukiwepo mradi wa ujenzi wa Bandaari ys Karema itakayo kuwa inatumiwa na Wananchi wa Tanzania na Nchi ya Kongo kwaajiri ya abiria na kusafirishia mizigo.


Kwa  mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko mbele ya Wandishi wa Habari ziara hiyo inatarajia kunza Agosti 25 hadi  Agosti 27.

Amebainisha kuwa ziara hiyo ya siku tatu inalengo ya kukagua  miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali katika Mkoa huu

Ameitaja miradi miradi itakayo tembelewa na Waziri Mkuu Kassim Majali ni  mradi wa  bandari ya Karema inayoendelea kujengwa na inatarajia kukamilika hivi karibu ziara  ya kutembelea Bandari hiyo itafanyika Agosti 25 ambayo ndio siku ya kwanza ya ziara yake

 Amesema siku ya tarehe 26 atazindua kiwanda cha usindikaji wa pamba katika Kijiji cha Ifukutwa Wilaya ya Tanganyika na  kisha ataelekea Mishamo kwenye makazi ya   Mishamo ambako atakagua ujenzi wa kituo cha Afya cha Mishamo 

  Siku ya tatu ambayo ndio  ya mwisho ya ziara yake Waziri Mkuu atatembelea kukagua ujenzi wa Hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi na kisha  akiwa njiani kuelekea Mkoani Tabora atakagua baraba ya kiwango cha lami inayoanzoa Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi hadi Mkoani Tabora .

 Amewataka wananchi wajitokeze kwa wingi  kwenye maeneo yao kwa kujipanga barabarani kwa kuzingatia tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa Corona

 Amesema kuwa kutokana hali  iliyopo kwa sasa  nchini ya tahadhari ya ugonjwa wa Corona kwenye ziara hiyo hakutakuwa na mikutano ya adhara .

 Mrindoko amewaomba wakazi wa Mkoa huu kuwa watulivu kwenye kipindi hicho cha  ugeni huu mkubwa na pia wananchi wajitokeze kwa wingi huku wakiwa wamepeana nafasi ya mita moja moja.

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages