![]() |
| Mratibu wa Mradi wa FISH4ACP wa Mikoa wa Katavi,Rukwa na Kigoma Hashimu Muumin,Akizungumza na wanahabari pamoja na wananchi wa Ikola Wilaya ya Tangayika Mkoa wa Katavi wa Mwaloni wa Ikola ziwa Tanganyika wakati akitamburisha mradi huo na malengo yake. |
Na George Mwigulu,Tanganyika.
Wananchi wa Mkoa wa Katavi wamehimizwa kuendelea kutunza na kusafisha fukwe za ziwa Tanganyika ili kulinda uhai wa viumbe vilivyo ndani ya ziwa ikiwa na kufanya uvuvi salama ili epuka kuwa sehemu ya kuchafua mazingira.

Kwa mujibu wa utafiti iliyofanywa na mradi wa kuimarisha uvuvi (FISH4ACP)ambao ni mpango wa jumuiya ya nchi za Afrika,Karibiani na Pasifiki(OACPS) unaonyesha kuwa ziwa Tanganyika kina chake kimepungua kutokana na shughuri za kibinadamu zinazofanywa ndani na nje ya ziwa hasa zinazoambatana kuchafua fukwe na mwalo.
Hashimu Muumin,Mratibu wa Mradi wa FISH4ACP katika mikoa ya Kigoma,Rukwa na Katavi alisema hayo hivi karibuni katika kijiji cha Ikola walaya ya Tanganyika Mkoani hapa wakati akitaburisha mradi huo wa miaka mitano uliombatana na kufisha fukwe na mwalo wa Ikola katika ziwa hilo.
![]() |
| Baadhi ya wananchi wa Ikola wakiwa katika mwaloni wa Ikola ziwa Tangayika kwenye jukumu la kusafisha mwalo huo,Zoezi hilo limeongozwa na mradi wa FISH4ACP. |
Muumin amefafanua malengo ya kujitokeza kusafisha fukwe na mwalo wa Ikola kuwa ni mwendelezo wa wiki ya kusafisha fukwe ambapo wanaungana na watu wengine wa ulimwenguni ili kuisafisha fukwe zetu ambazo zimeelemewa sana taka za plastiki ,taka ngumu ambazo zinaingia kwenye maeneo ya uvuvi.
![]() |
| Baadhi ya wananchi wa Ikola wakiwa katika mwaloni wa Ikola ziwa Tangayika kwenye jukumu la kusafisha mwalo huo,Zoezi hilo limeongozwa na mradi wa FISH4ACP. |
![]() |
| Anthony Daudi kijana Mkazi wa Kijiji cha Ikola ambaye ameamua kujitokeza kufanya usafi katika mwalo wa Ikola ziwa Tanganyika pia amesema kuwa amewashukuru FISH4ACP kwa mradi ambao umewaamsha kutoka usingizini kwa kutokutambua wajibu wao wa kusafisha fukwe na mwalo huo. |
" ...wananchi madhara ya kuchafua fukwe na mwalo ni makubwa kwa kuwa yanasababisha upungufu wa samaki na kusababisha matatizo katika maeneo yetu ya mavuvi kwa sababu taka zinazuia miale ya jua kuingia kwenye maeneo ya maji au vyanzo vya maji " Alisisitiza Mratibu huyo.
![]() |
| Afisa Uvuvi wa Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi,Donald Kusekwa akizungumzia juu ya mradi wa FISH4ACP na namna ambavyo kama serikali inashiriki katika masuala ya kuhakikisha fukwe na mwalo zinakuwa kwenye usafi |
Afisa Uvuvi wa halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi Donald Kusekwa licha ya kushuru mradi huo amebainisha kuwa hali ya fukwe hapo awali za ziwa Tanganyika hazikuwa za kuridhisha na sasa wanaona mazingira niyakupendeza.
Kusekwa amesema hamasa iliyotolewa na mradi wa FISH4ACP kwa wananchi ni kubwa kwani umechangia wananchi kuona umuhimu wa kusafisha na kutunza fukwe na mwaloni kwa ajili ya faida yao na taifa,Hivyo kama serikali wataendelea kushirikiana na mradi huo.
![]() |
| Bi Salma Jumanne Mkazi wa Ikola akielezea namna ambavyo wamepokea mradi wa FISH4ACP kuwa umeleta hamasa ya kuhamsika kufanya usafi. |





