TRA YATOA SHAKA WAFANYABIASHA KWA KUENDELEA KUKUSANYA KODI KWA NJIA YA MAELEWANO.


    Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa mlipa kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Makao Makuu,Richard Kayombo.

Na George Mwigulu,KTPC Katavi.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewahakikishia wafanyabiashara wote nchi kuwa itaendelea kukusanya mapato ya kodi kwa kuzingatia maelekezo yaliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassain ya kukusanya mapato kwa njia ya maelewano kinyume na nguvu ili wafanya biashara waendelee kuiona TRA ni rafiki na sio adui wao.

Richard Kayombo,Mkurungezi wa huduma na elimu kwa walipa kodi wa TRA Makao Mkuu amebainisha hayo katika Ukumbi wa polisi,Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wakati akifungua semina ya kuwajengea uelewa wa kulipa kodi kwa wafanyabishara mkoani hapa.

Semina hiyo ya siku moja ziliwasilishwa mada mbalimbali ikiwemo ya mabadiliko ya sheria za kodi kwa mujibu wa sheria ya fedha ya mwaka 2021,Kupanua wigo wa kodi na kuleta usawa katika sekta ya kilimo kwa kuzingaitia sheria ya kodi ya ongezeko la thamani na mabadiliko ya sheria ya VETA 82.

Mkurugenzi huyo aliwasisitiza wafanyabiashara kufanya biashara zao  kwa kufuata taratibu na kutekeleza wajibu wao wa  kulipa kodi kwa wakati  na  wahakikishe wanapomuuzia mtu bidhaa wanampatia risti kwani inakuwa inasaidia  makusanyo kupatikana kwa haki .

Kayombo alifafanua kuwa lengo la mamlaka hiyo sio  kuwatoza watu faini  wafanya biashara wanaoshindwa kulipa mapato kwa wakati hivyo kama wanataka wafanya biashara kuondokana na faini hizo wanatakiwa kutimiza wajibu wao kwa kulipa kodi kwa  wakati .

Alibainisha kuwa  wafanyabiashara wanapo lipa kodi kuna saidia serikali kuwaletea wananchi  huduma muhimu za kijamii na ndio maana  maeneo mengi  yanayofanyiwa kazi  na serikali  yanayohusu  kodi mbalimbali  yanazingatia maoni ya wafanyabiashara

“ maboresho yanayofanywa na serikali kuhusu kodi yanazingatia maoni ya wafanyabiashara na yanawanufaisha kwa asilimia 70 hivyo kutokana na marekebisho hayo inaonesha jinsi gani serikali inavyofanya kazi zake kwa kushirikiana  kwa ukaribu zaidi ndio maana wafanyabiashara wanayo haki ya kusikilizwa  pindu wanapokuwa hawajaridhika na kodi” alisema Kayombo.

Isihaka Shariff, Afisa Msimamizi wa Kodi Idara ya elimu na huduma kwa mlipa kodi kutoka TRA akiwasilisha mada mbalimbali kwenye semina hiyo alisema hivi karibuni serikali imefanya  maboresho ya sheria  mbalimbali za kodi.

Afisa Msimamizi wa Kodi idara ya elimu na huduma kwa mlipa kodi,Isihaka Sharrif.


Afisa huyo alisema baadhi ya  maboresho hayo ni sheria ya kodi ya ongezeko la thamani  ambapo mabadiko yamefanyika kwenye kifungu cha tatu  yamefanywa kuwa kifungu kidogo cha kwaza,Vifungu vipya vimeongezwa  2,3 na 4 ambavyo vinaeleza kama VAT kwa bidhaa imelipwa Zanzibar kwa kiwango ambacho ni sawa na Tanzania bara ,basi bidhaa hiyo itachukuliwa imelipiwa kodi na haitatozwa tena kama itakaposafirishwa kwenda Tanzania bara.

Shariff alielezea kuwa ikiwa bidhaa imelipwa VAT Zanzibar kwa kiwango pungufu ukiliiinganisha na Tanzania bara,bidhaa hiyo ikihamishiwa bara,tofauti ya kiwango hicho cha VAT itakusanywa Tanzania bara.

“ naombeni mtambue ikiwa bidhaa imezalishwa Tanzania bara na kuuzwa kwa mtu aliyesajiliwa na VAT Zanzibar,kodi itakusanywa na TRA kwa niaba ya ZRB na kuirejesha kwa ZRB” alisisitiza Shariff.

Aidha  serikali imefanya  maboresho ya sheria  ya kwa baadhi ya  vitu  baadhi ya vitu hivyo ni  bidhaa mitaji , maboresho ya  kusamehe  vifaa vya  kubebea maziwa , wamesamehe  vifungashio  vya madawa  pia wamesamehe kodi ya simu za simu janja  ili watanzania wengi  waweze  kunufaika na simu hizo .

 Mwenyekiti wa Jumui ya Wafanya biashara Tanzania Tawi la Mpanda Amani Mahella  aliwataka wafanya biashara  wawe waaminifu  kwa kufanya biashara zao pasipo kudanganya kwa lengo la kutaka kulipo kodi kidogo ambazo hazina uhalisia .

 Kwani kitendo cha mfanya biashara   kukwepa kulipa mapato  ni kitendo kibaya sana na wala hakina faida  bali kinakuwa kikimfanya mfanya biashara kuhatarisha biashara yake na ndio inaweza kumfanya asiendelee tena kufanya biashara kwani anaweza hata kukosa mtaji.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages