NYUMBA KUMI ZA CHOMWA MOTO MKOA WA KATAVI

 

Kaimu  Kamanda wa Polisi  Mkoa wa Katavi  Silvester Ibrahimu akitoa Taarifa ya Matukio mbalimbali mbele ya Waandishi wa Habari

Na  Walter Mguluchuma

    Katavi 

Nyumba kumi katika Kijiji cha Igongwe Kata ya Sitalike Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi  zimechomwa moto na kuteketea pamoja na kuharibu mali zilikuwemo ndani ya nyumba hizo ikiwemo chakula.

Kaimu Kamanda wa  Polisi Mkoa wa Katavi Sylvester Ibrahimu  alisema nyumba hizo kumi zilikuwa  zikimilikiwa na Sayi  Wema na Nyamizi Luhemela  wakazi wa Kijiji cha Igongwe.

Ameeleza kuwa  thamani ya mali hizo zilizoteketea kwa moto ikiweo mahindi na mpunga bado hazijafahamika ambapo  katika tukio hili watuhumiwa  nane wamekamatwa kuhusika na tukio hili .

Ambao amewataja kuwa ni  Daud  Gembe , Abasi  John, Ginius Sindani , Julius Nicholaus, Godfrey   Basili( MASAGA), Joseph   Lepard, Kilisen  Mwananjela  wote wakazi wa Kijiji cha Sitalike na  Japhari  Razaro  mkazi wa Kijiji cha Vikonge Wilaya ya Tanganyika .

Kamanda Ibrahimu alisema  katika tukio hilo mtuhumiwa mmoja  aitwaye Vicenti Mwananjela  amefariki dunia  wakati alipokuwa akipatiwa matibabu  katika Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa wa Katavi   kutokana na   wananchi kujichukulia sheria  mikononi kwa kumshambulia kwa kumpiga baada ya kuhusika kwenye tukio hilo la kuchoma nyumba moto .

Alisema watuhumiwa  hao wanaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi kuhusiana na tukio hilo la kuchoma nyumba hizo moto na upelelezi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani .

Kaimu  Kamanda  amesema Jeshi hilo pia limewakamata watu saba wanaodaiwa kujichukulia sheria  kwa kumpiga hadi kumuuwa mtuhumiwa   Klisent  Mwananjela  aliyekuwa  anatuhumiwa na watuhumiwa wengine saba kwenye tukio la kuchoma nyumba hizo kumi Moto.

 

 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages