PREMIUM YATOA MSAADA WA USAFIRI UTAKAO SAIDIA KUZUIA UHALIFU

Yusuph Mahundi Meneja  Mahusino na usimamizi wa  Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA akimkabidhi kadi ya Pikipiki Mkuu wa kituo cha Polisi mishamo.

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Kampuni  ya  ununuzi  wa Tumbaku ya PREMIUM  ACTIVE TANZANIA imetoa msaada  wa  usafiri  wa Pikipiki kwa kituo  cha Polisi cha Mishamo  katika Mkazi ya wakimbizi Mishamo  Wilaya ya Tanganyika  Mkoa wa Katavi utakaosaidia shughuli mbambali za kuimarisha usalama kwenye eneo hilo.

Mkuu wa kituo cha Polisi Mishamo Andrea Msesemi kushoto akitoa shukrani zake kwa kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA kwa kuwapatia usafiri wa Pikipiki. 

Kampuni  ya  ununuzi  wa Tumbaku ya PREMIUM  ACTIVE TANZANIA imetoa msaada  wa  usafiri  wa Pikipiki kwa kituo  cha Polisi cha Mishamo  katika Mkazi ya wakimbizi Mishamo  Wilaya ya Tanganyika  Mkoa wa Katavi utakaosaidia shughuli mbambali za kuimarisha usalama kwenye eneo hilo.

Msaada huo wa  pikipiki ya kisasa  yenye thamani ya zaidi ya shilingi  Milioni nne  umekabidhiwa na Meneja uhusiano na usimamizi wa Kampuni ya Premium Tanzania aliyekabidhi kwa niaba ya Kampuni hiyo .

Mahundi akikabidhi pikipiki  hiyo yenye ukumbwa wa CC 250 amesema  wao kama kampuni ya Premium walipokea ombi kutoka   Jeshi la polisi  Mkoa wa Katavi kwa ajiri ya kituo cha polisi cha  mishamo .

Kuitokana na ushirikiano ambao wamekuwa wakiupata katika shughuli zao za ununuzi wa Tumbaku  kwenye eneo hilo  na  kwa Mkoa wa Katavi  kutoka kwa wadau  mbalimbali na Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi.

Hivyo waliona  ni jambo njema sana  wao kama kampuni ya Premium Active  Tanzania  kuweza kusaidia kwenye swala la usafiri ambao utasaidia kuwezesha swala la usafiri kwa  kituo cha Polisi Mishamo .

Mwakilishi wa Mkuu wa Makazi  ya  Mishamo  Jimmy Molle  amesema  wao kama ofisi ya Mkuu wa Makazi ya wakimbizi ya Mishamo wamefurahi sana kuona  kituo cha Polisi kinakabidhi  wa usafiri wa pokipiki ya kisasa na imeonyesha jinsi ambavyo kampuni ya Premiun inavyo wajari na inavyorudisha  fadhila kwenye jamii.

Amebainisha kuwa kituo hicho cha Polisi kulikuwa na changamoto  kwani usafiri wao ulikuwa umechakaa  hivyo pikipiki hiyo itasaidia sana kuimalisha usalama kwenye maeneo  yao   kwa kuhakikisha  yanakuwa salama zaidi .

Meneja Uhusiano na usimamizi wa Kampuni ya PREMIUM ACTIVE TANZANIA Yusuph Mahundi Katikati akielezea namana kampuni hiyo inavyoguswa na masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo wanayofanya biashara ya unununuzi wa zao la Tumbaku kwenye Mkoa wa Katavi.
Molle ameeleza kuwa   pia  itasaidia  wadau wao  hasa wakulima wa Tumbaku  kuzuia baadhi ya wakulima ambao walikuwa sio waaminifu kwa    kutorosha tumbaku kwenda sehemu nyingine kwa lengo la kukwepa deni  la pembejeo .

Mkuu wa   Kituo cha Polisi  Mishamo  Andrea  Msesemi amesema  anatoa shukurani  za dhati kwa Kampuni ya Premium kwa msaada huo muhimu kwa Jeshi la polisi  kwa kuweza kukubali kupokea maombi yao .

Amesema wao kama polisi wataendelea kuwatambua kampuni  hiyo kama wadau wao mhimu  ambao wameweza kuwapatia chombo cha usafiri  kwa jeshi la polisi Mishamo itakayo wasaidia kuweza kupambana na uhalifu na wahalifu .

Amefafanua kuwa kwani itawasaidia kwenye dolia zao  wanazofanya kila siku  kutoka kijiji kimoja  kwenda kijiji kimgine kutoka na  eneo hilo la ,makazi kuwa na eneo kubwa  hivyo itawasaidia sana .

Amesema kwa ujumla  anaishukuru kampuni ya Premium kwa Msaada huo huku akiiomba kampuni hiyo kuendelea kuwa wadau mhimu wa ulinzi na usalama kwa kutoa pikipiki ili kuimarisha ulinzi wa Raia na Mali zao.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages