ZAIDI YA BILIONI 2.3 YA MIRADI YA MAENDELEO KUFUATILIWA NA TAKUKURU MKOA WA KATAVI


Mkuu wa Takukuru  Mkoa wa Katavi Festo  Mdede akitowa taarifa kwa Waandishi wa Habari   juu ya utekelezaji wa kazi wa Takukuru Mkoa wa Katavi  ambapo wameweza kufanya uchunguzi kwenye miradi ya maendeleo ya zaidi ya Bilioni 2.3(Picha na Walter MguIuchuma)

  Walter Mguluchuma,Katavi .

Takukuru  Mkoa wa Katavi  katika pindi cha miezi mitatu ya kuanzia Januari hadi Machi mwaka huu imefanya kazi  ya kufatiliaji wa fedha  za utekelezaji  wa miradi  ya Maendeleo saba  yenye  thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 2.3.

Hayo yasemwa na  Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi  Festo Mdede  wakati alipokuwa akitowa taarifa ya utekelezaji wa Takukuru mbele ya Waandishi wa Habari kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Machi  mwaka huu.

Alisema  Takukuru  wamefanya  kazi ya ufatiliaji  wa fedha za  utekelezaji  wa miradi ya Maendeleo  saba yenye  jumla ya  thamani  ya shilingi  2,346,844,793 vilevile wamefuatilia ujenzi  wa vyumba  vya madarasa  vya shule za sekondari  na vituo shikizi  namba 5,441 chini ya mpango  wa maendeleo  na Ustawi  wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO 19.

Fedha hizo  zilitolewa na  Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia  Suluhu Hassan  kupitia mpango  huu Mkoa wa Katavi  ulipokea  jumla ya  sh Bilioni  8,580,000,000.

Alibainisha kuwa  lengo la ufatiliaji  huo ni kuangalia  iwapo  kuna mianya ya Rushwa kwenye utekelezaji  wa miradi  na kuongeza uwazi  na upatikanaji wa  thamani  ya fedha za miradi ya Serikali.

Mdede  alieleza kuwa  katika kusimamia miradi hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi  aliunda timu za ufuatiliaji  katika maeneo yote ya Halmashauri za Mkoa wa Katavi  katika ufuatiliaji huo  ukiukwaji  wa taratibu  katika kukamilisha miradi ulibainika .

Alizitaja kasoro zilizobainika kwenye miradi hiyo kuwa ni  wizi wa vifaa  vya ujenzi,matumizi mabaya ya fedha za  miradi ,ujenzi kutokamilika kwa wakati na baadhi ya thamani kutengenezwa  chini ya kiwango .

Mkuu huyo wa Takukuru  Mkoa wa Katavi alisema  baada   ya ubainishwaji  wa makosa hayo Takukuru  ilichukua hatua stahiki  ikiwa ni pamoja  na kutoa  maelekezo  kwa  waliotengeneza thamani  za shule  chini ya kiwango kurudia utengenezaji kwa gharama zao binafsi .

Pia kuanzisha uchunguzi  kwa makosa mengine ya wizi  na  vifaa vya ujenzi  na matumizi  mabaya ya fedha  za miradi ili hatua stahiki zichukuliwe.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages