UJENZI WA DARAJA LA THAMANI YA BILIONI MBILI KUINUA UCHUMI WA KATAVI NA KIGOMA.

Baadhi ya wataalamu ambao wako wanafanya tathimni wa kiufundi namna ambavyo daraja hilo litakavyojengwa.

 Na Walter Mguluchuma,Tanganyika .

WAKAZI wa Mishamo   Wilayani Tanganyika  Mkoani   Katavi wataondokana  na changamoto  ya muda mrefu ya kusafiri umbali mrefu kwa kutumia baiskeli  au kutembea kwa miguu kwenda kununua samaki na mafuta ya mawese katika mwambao wa Ziwa Tanganyika baada ya ujezi wa daraja la kuuganisha mkoa wa Kigoma kuanza kujengwa.


Wakazi wa Mishamo   Wilayani Tanganyika  Mkoani   Katavi wataondokana  na changamoto  ya muda mrefu ya kusafiri umbali mrefu kwa kutumia baiskeli  au kutembea kwa miguu kwenda kununua samaki na mafuta ya mawese katika mwambao wa Ziwa Tanganyika baada ya ujezi wa daraja la kuuganisha mkoa wa Kigoma kuanza kujengwa.

Kujengwa kwa daraja na barabara hiyo kutakuwa ni  mkombozi wa wananchi wa Mikoa ya Katavi na Kigoma katika kuinua uchumi wa wananchi hao na taifa kwa ujumla .

Meneja wa Wakala wa  Barabara  Tanzania(TANROADS) Mkoa wa Katavi,Mwandisi  Martini  Mwakabende  amesema kuwa   daraja hilo kubwa la aina yake litagharimu kiasi cha shilingi Bilioni mbili.

Amebainisha kuwa katika  katika ujenzi wa madaraja yaliyojengwa na kusimiwa na TANROADS  Mkoa wa Katavi hilo ni daraja la pili kwa ukubwa  na lililotumia gharama ya fedha nyingi daraja la kwanza ni la mto  Koga linaloiunganisha Mikoa ya Katavi na Tabora .

Amesema kuwa ujenzi wa daraja hilo unatarajiwa kukamilika mwezi wa pili mwakani 2023 na mradi huu unatekelezwa na Kampuni ya ujenzi ya   MSELEM CIVIC ENG  CONST y a  Mkoani  Rukwa.

Msimamizi wa ujenzi wa  daraja hilo kutoka kwenye Kampuni hiyo Uwesu  Salum Uwesu ameeleza  kuwa licha ya kipindi cha masika  kuwa karibu uanze  wanatarajia kumaliza mradi huo kwa wakati .

Mkazi  wa Mlibasi  Evaristi  Noribo alisema kuwa  kukamika kwa daraja hilo itakuwa ni mkombozi mkubwa kwa wananchi wa Mishamo walikuwa wakilazimika kutembea kwa miguu kwa muda wa siku mbili hadi kufika mwambao mwa Ziwa Tanganyika  kwa ajiri ya kufatia samaki ,dagaa na mafuta ya mawese.

Amesema kuwa yeye ameishi kwenye eneo la Kijiji hicho toka mwaka 1975 hivyo anaona ni kama ndoto kujengwa kwa daraja hilo muhimu kwa uchumi wa wananchi wa mikoa ya Katavi na Kigoma

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages