Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizungumza na watumishi mbalimbali wa idara ya maji Manisipaa ya Mpanda wakati akikabidhi pikipiki kwao zenye jumla ya thamani ya Mil 99 |
Na Paul Mathias,Mpanda.
Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira Muwasa Katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa katavi imepatiwa pikipiki 30 na Serikali Zenye Samani ya shilingi Milion 99.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akizindua zoezi la ugawaji wa pikipiki 30 kwa wataalamu mbalimbali wa idara ya maji Manispaa ya Mpanda. |
Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira Muwasa Katika halmashauri ya Manispaa ya Mpanda mkoa wa katavi imepatiwa pikipiki 30 na Serikali Zenye Samani ya shilingi Milion 99.
Akikabidhi
pikipiki hizo kwa niaba ya Serikali katika hafla iliyofanyika Ofisi za Muwasa
Manispaa ya Mpanda mkoa wa katavi Mkuu wa Mkoa Katavi Mwanamvua Mrindoko
amesema pikipiki hizo zikatumike kwa lengo lililokusudiwa ili kuendelea kutoa
huduma kwa wanachi nasio kwenda kufanyia Shughuli Binafsi.
Mwanamvua
amesema katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma mbalimbali kwa muda
unaotakiwa Serikali ya awamu ya Sita Chini ya Rais samia Suluhu Hassan imekuwa
ikiendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wafanyakazi kwa kuwapatia vyombo vya
Usafiri kama pikipiki na vifaa vingine kwa Madhumuni ya kuimalisha ufanisi wa
kazi kwa Wafanyakazi.
Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko akikabidhi funguo za pikipiki kwa mlengwa Christina Mbula. |
Katika hatua nyingine Mwanamvua amesema amekuwa anapokea malalamiko kutoka kwa wananchi ya kubambikiziwa Bili za maji kwa wateja kutoka mamlaka ya Muwasa na kuwaomba kutumia pikipiki hizo zilizotolewa na serikali kuwafikia wateja wao kwa Kusoma Mita zao kwa wakati ili kupunguza malalamiko hayo kwa wateja wao.
Katika
hafla hiyo amesisitiza Utaratibu wa Mgao wa Maji kusimamiwa kwa utaratibu
unaoeleweka na kusiwepo na aina yeyote ya kwenda kinyume na Utaratibu wa Mgao
huo wa Maji hali amabayo huwaathili watumiaji wa huduma hiyo kwa kukosa Huduma
hiyo kwa wakati.
Mkuu
huyo wa mkoa ametoa Rai kwa wananchi kuendelea kutunza vyanzo vya Maji kwani
uwepo wa vyanzo hivyo ndio unafanya huduma ya maji kupatikana kwa wananchi na
Kuziomba mamlaka zinazohusika na masuala ya uhifadhi kuendelea kusimamia
kikamilifu sharia zinazo husu Usimamiaji wa Uhifadhi wa mazingira na Misitu
katika mkoa wa katavi.
Awali akisoma Taarifa ya Mamlaka ya Maji safi na usafi wa Mazingira [MUWASA] Mkurugenzi wa mamlaka hiyo Manispaa ya Mpanda Eng Hussein Nyemba amesema anaishukuru wizara ya Maji kwa kuwapatia pikipiki hizo amabazo zitasaidia kulinda Vyanzo vya Maji,pamoja na kuhudumia wateja kwa haraka na kusaidia kuziba Mivujo ya Maji na kuizibiti kwa haraka.
Mkurugenzi wa MUWASA,Eng Hussein Nyemba akitoma taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanmvua Mrindoko. |
Nyemba
amebainisha kuwa kuwa vyombo hivyo vya usafiri vitasaidia katika ukusanyaji wa
Mapato kwa Taasisi hiyo na kuisadia katika makusanyo ya Maduhuri ya serikali
kwa haraka tofauti na ilivyokuwa hapo awali.
Ameongeza
kuwa katika kuhakikisha sharia za usalama barabarani hazikiukwi kwa Maafisa
waliopewa Pikipiki hizo walipewa elimu juu ya sheria za usalama barabarani kwa
kushirikiana na ofisi ya kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi ili watumishi hao
watumie vyombo hivyo kwa usitadi unaotakiwa kwa kuzinagatia sharia za usalama
barabarani.
Nao
baadhi ya watumishi waliopatiwa pikipiki hizo akiwemo Bwana Lema Jeremia
Meneja ufundi Muwasa amesema wanamshuru Rais Samia suluhu hassan kwa kutatua
changamoto ya usafiri ambayo imekuwa ikiwasumbua kwa muda Mlefu hali
iliyopelekea kuwa na changamoto kubwa ya utendaji kazi za kila siku.
Jeremia
amebainiha kuwa walikuwa wanachelewa kuwahudumia wateja wao kwa kuchelewa
kufika kwenye Mivujo ya maji na kuiziba kwa wakati huku ujio wa pikipiki hizo
utakuwa mkombozi kwao na watafanya kazi kwa bidii.