TAKUKURU YABAINI DOSARI YA MIRADI YA THAMANI YA BIL2.1 MKOANI KATAVI.

 

Naibu Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stuart Kiondo akitoa taarifa ya utendaji kazi kwa umma mbele ya Waandishi wa Habari [PICHA na Paul Mathias]

Na  Walter Mguluchuma,Katavi

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi  imebaini  kuwepo kwenye miradi   iliyotekelezwa  katika Halmashauri mbambali za Mkoa huu ikiwa na upungufu wa Zaidi ya Shilingi Bilioni 2.1 na wameweza kuchukua hatua mbambali  kwenye miradi hiyo .

Waandishi wa Habari mkoa wa Katavi wakiwa katika majukumu yao wakati taarifa ya utendaji kazi ya Takukuru ikitolewa ofisini hapo[Picha na Paul Mathias]

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na  Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi  imebaini  kuwepo kwenye miradi   iliyotekelezwa  katika Halmashauri mbambali za Mkoa huu ikiwa na upungufu wa zaidi ya Shilingi Bilioni 2.1 na wameweza kuchukua hatua mbambali  kwenye miradi hiyo .

Hayo yamesemwa na Naibu Mkuu wa Takukukuru  Mkoa wa Katavi  Stuart  Kiondo  wakati alipokuwa akitowa taarifa kwa wandishi wa Habari ya utekelezaji  wa kazi wa Taasisi hiyo kwa kipindi cha miezi mitatu yakuanzia Oktoba  hadi desemba 2022.

Amebainisha kuwa  Takukuru Mkoa wa Katavi katika kipindi hicho cha miezi mitatu  ya October na Decembe Mwaka 2022 wameweza kufatilia  miradi yenye  thamani  ya shilingi  Bilioni  5 katika  sekta  za ujenzi,elimuna afya .

Katika ufatiliaji huu wa miradi kwenye Mkoa huu  wameweza kubaini miradi yenye thamani  Sh,2,170,000,000 ikiwa na mapungufu kwenye miradi iliyotekelezwa katika Halmashauri mbambali za Mkoa huu.

Kiondo  amesema  kati ya shilingi Bilioni 5 zilizotolewa kati hiyo shilingi Bilioni  1. 12 zilitolewa na  Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan zijulukanazo  Pochi la Mama .

Waandishi wa habari mkoa wa Katavi wakisikiliza Taarifa ya utendaji kazi wa Takukuru ofisini hapo[Picha na Paul Mathias]

Fedha hizo ambazo  zilitumika kujengea  jumla ya madarasa  55katika  shule  25 madarasa ambayo yamekamilika  na yameanza kutumika .

Naibu Mkuu huyo wa Takukuru ameitaja baadhi ya miradi hiyo  ni  miradi  yenye upungufu ni mradi wa  ujenzi wa  jingo  la  ICU na nyumba  za watumishi  Hospitali ya Wilaya ya Tanganyika  yenye thamani y ash,340,000,000 miradi hiyo ilikutwa na  mapungufu  yakuweka matofali yasiyo na kiwango na ukiukwaji wa  taratibu  za manunuzi  na tayari uchunguzi umeanza .

Uujenzi wa kituo cha Afya Itenka  Halmashauri ya Nsimbo wenye thamani ya  wenye thamani y ash ,530,000.000,ujenzi  wajengo   la dharura  Hospitali ya Halmashauri ya Nsimbo  sh 300,000,000 na ujenzi  wa majengo matano  Bohari , mionzi  jingo la utawala , jingo la mama na mtoto  na jingo la kufulia nguo yenye thamani y ash 1,000,000,000 Hospitali ya Nsimbo .

Amesema kasoro walizozibaini ni  ukiukwaji wa  taratibu  za manunuzi  na ucheleweshaji ambapo uchunguzi wake tayari umeanza  na waliweza  kubaini matofali  matofali yalitumika kwenye ujenzi hayakuwa  na ubora baadhi ya kuthibishwa .

Naibu mkuu wa Takukuru Mkoa wa Katavi Stuart Kiondo akizungumnza na waandishi wa Habari juu ya utendaji kazi wa Takukuru Mkoa wa Katavi kwa kipindi cha October hadi December 2022[ Picha na Paul Mathias]

Kiondo ameeleza kuwa  katika kipindi cha  robo ya kipindi cha  Januari  hadi Machi mwaka huu wanataraji kuongeza  juhudi  za kuimarisha  kuzuia rushwa  kwa kufatilia  utekelezaji  wa miradi  ya maendeleo  na kuhamasisha  kutoa elimu  kwa wananchi  ya ushiriki  wa kupiga vita rushwa .

Na wataendelea  kufatilia  kwa karibu  fedha  zote  zinazotolewa na  Serikali  ili kuhakikisha  zinatumika  kama ilivyokusudiwa  na upande  wa miradi  kuwa bora  na thamani ya fedha kuonekana .

Kiondo amewataka wananchi wa Mkoa wa Katavi kutoa taarifa mara moja pindi ambapo wanapokuwa wanapigiwa simu na watu ambao   ni matapeli wanao kuwa wamewapigia simu na kujifanya wao ni Maafisa wa Takukuru kwa lengo la kuwatishia na kutaka kujipatia pesa.

kwa habari zaidi tembelea ukurasa wetu wa 

https://kataviclub.blogspot.com/

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages