WADAU WA SALAMU MLELE WATEMBELEA KITUO CHA AFYA

 

Wanachama wa umoja wa watuma salamu Wilaya ya Mlele wakiwa katika kituo cha afya Inyonga kwaajili ya kuwafariji wagojwa.

Umoja wa watuma salamu katika halmashauri ya wilaya ya mlele mkoa wa katavi wametembelea kituo cha afya cha Inyonga B wamefanya matendo ya huruma kwa kuwatembelea wagojwa na kuchangia damu kama ishara ya upendo katika kipindi hiki cha Mfungo wa kwarezima.

Mwenyekiti wa umoja wa watuma salamu wilaya ya mlele Maganga peter amesema kuwa wao kama watuma salamu wamewiwa kufanya matendo ya huruma kwa kuwaona wagojwa hao hospitalini hapo

‘’mimi nimeona nivyema sana kama mwenyekiti wa salamu klabu wilya ya Mlele kwa sababu huu ni mwezi wa kwarezima lakini pia tunaenda mwezi wa ramadhani,unapotoa kitu unajiwekea akiba kwa mwenyezi Mungu kwa sababu ni mwezi wa toba wagojwa wamefarijika kwa kile tulichojaliwa kuwapatia’’amesema Maganga

Pius kipeta Mwenyekiti wa Katavi salamu club amesema kuwa jamii ijenge umuhimu wa kuwatembelea wagojwa na kuwafaliji kwakuwa Maradhi kwa mwanadamu nisehemu ya maisha hivyo kila mmoja anaowajibu wa kuwafariji wagojwa kwa kadri alivyojaliwa.

‘’tumeamua kuleta tabasamu kwa hiki unakuta wengine wanaumwa kwa muda mrefu unakuta wanajikatia tamaa lakini wakiona jamii inawatembelea wanafarijika ‘’

Mganga mfawwidhhi wa kituo cha afya Inyonga Gilishi Jonh  amewashukuru watuma salamu hao kufika hospitalini hapo kwa kuja kuwafariji wagojwa.

 Wanachama wa umoja wa watuma salamu wamesema wataendelea kuwa karibu na jamii ili kuonyesha upendo kwakuwa wao ni sehemu ya jamii ya wanatania.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages