RC: KATAVI TUNATAMBUA MCHANGO WA WAANDISHI WA HABARI


Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akiwasili katika ofisi za Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Katavi
Na Paul Mathias-Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewaagiza wakuu wa  idara za Serikali  katika Mkoa wa Ktavi  kuhakikisha wanatoa ushirikiano  kwa wandishi wa Habari  wanapokuwa katika Majukumu yao 

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko aliekaa katikati akiwa katika picha ya pamoja na Waaandishi wa habari mkoa wa katavi alipotembelea ofisini hapo

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko amewaagiza wakuu wa  idara za Serikali  katika Mkoa wa Katavi  kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari wanapokuwa katika majukumu yao ya kihabari.

Agizo hilo amelitoa wakati alipokuwa   akizungumza na wandishi wa Habari wa vyombo mbali mbali vya Habari vilivyoko katika Mkoa wa  Katavi kwenye ofisi ya Klabu ya  Wandishi wa Habari   Mkoa wa Katavi wakati wa  ziara yake  aliyoifanya. 

Mkuu wa mkoa wa Katavi mwanamvua Mrindoko akiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari Mkoa wa Katavi baada ya kutembelea ofisi za klabu ya waandishi wa habari mkoa wa katavi

Amesema  wandishi wa habari wanatakiwa kupata habari za kutoka idara Fulani wapewe ushirikiano mkubwa na waharaka ili waweze kutekeleza kwa wakati majukumu yao ya kuabalisha umma wa wana Katavi naWatanzania kwa ujumla yake .

Mrindoko ameeleza kuwa  wandishi wa habari wa Mkoa wa Katavi  wanafanya kazi kubwa ya kuutangazo Mkoa wa Katavi ndani ya Mkoa na nje ya Mkoa na wamekuwa wakifanya kazi kwa uzalendo mkubwa kwa  kujitoa bila kujali muda wala umbali wa eneo wanalokwenda kufanyia kazi.

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akabidhiwa  taarifa ya klabu ya waandishi wa Habari iliyosomwa na Paschal Katona katibu wa Klabu ya waandishi wa Habari mkoa wa Katavi. 
Amesisitiza kuwa  Serikali ya Mkoa wa Katavi itaendelea kutowa ushirikiano mkubwa  kwa wandishi wa habari ili waendelee kufanya kazi yao pasipokuwa na shida ya aina yoyote na kuhakikisha usalama wao unalindwa.

Kwa kutambua mchango wa wanndishi  yeye kama mkuu wa Mkoa  anawahidi kuwapatia pikipiki mbili ambazo  ambazo zitawasaidia  kuzitumia kwenda  kwenye maeneo na kuweza kufika kwa haraka kwenye matukio hasa kwenye maeneo ya pembeni mwa mji kwani kwa sasa wanalazimika kuwa wanatumia usafiri  wa kukodi hali ambayo imekuwa ikiwafanya washindwe kufika kwa wakati .

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko akisalimiana na waandishi wa Habari mkoa wa Katavi alipotembelea ofisi ya klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Katavi.
Akisoma risala ya Klabu ya waandishi wa habari Mkoa wa Katavi Katibu wa Klabu Pascal Katona amesema   wandishi wa Mkoa wa Katavi wataendelea  kuwahabarisha wananchi  wa Mkoa wa Katavi  na Watanzania  kwa ujumla  kuhusu shughuli mbambali za maendeleo zinazofanyika .

Mwenyekiti wa Chama hicho  Walter Mguluchuma amesema waandishi wa Habari wapo tayari kuendelea kufanya kazi  za kushirikiana na Serikali kwa lengo la kuhabarisha umma na kusaidia kuweza kuleta maendeleo ya kweli katika mkoa wa Katavi.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko ameahidi kutoa Pikipiki Mbili kwaajili ya klabu ya waandishi wa Habari pamoja na kutoa kiasi cha shilingi Milioni Mbili kwaajili ya kusaidia klabu ya waandishi wa habari katika mkoa wa Katavi.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages