DC AHIMIZA KULINDA TUNU YA AMANI

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akiongoza kikao cha kamati ya amani na maridhino Wilaya ya Mpanda chenye lengo la kudumisha amani.

 Na Abdi Lunyamila -Mpanda
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameiomba kamati ya Amani na Maridhiano ya Wilaya ya Mpanda kuendelea kuhubiri amani na utulivu kwenye taasisi wanazoziongoza ili kudumisha umoja na mshikamano kwenye jamii.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph ameiomba kamati ya Amani na Maridhiano ya Wilaya ya Mpanda kuendelea kuhubiri amani na utulivu kwenye taasisi wanazoziongoza ili kudumisha umoja na mshikamano kwenye jamii.

Akizungumzakwenye kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu huyo wa wilaya Jamila amesema kuwa wakati wa kampeni na wakati wa uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 29 Oktoba 2025 Wilaya ya Mpanda haikuathirika na Vurugu ya aina yeyote.

 “Ndugu viongozi tutakumbuka kuwa Wilaya yetu ya mpanda haikupata taharuki wala aina yoyote ya vurugu kabla ya kampeni,wakati wa kampeni wakati wa Uchaguzi na hata baada ya Uchaguzi tofauti na baadhi ya maeneo mengine hapa nchini’’DC Jamila

Amewashukuru viongozi wa Dini kwa mshikamano sala pamoja na dua kuiombea Wilaya ya Mpanda kuwa na Amani, kabla ya uchaguzi na baada ya uchaguzi .

 “nitumie nafasi hii kuwapongeza na kuwashukuru viongozi wote viongozi wa Dini,viongozi wa vyama vya siasa walioko hapa,waandishi wa Habari na Wananchi wote wa Mpanda kwa Umoja wao kwa sala na dua lakini umoja na mshikamano nao umesababisha kuleta Amani katika Wilaya yetu ya Mpanda” Amesema Jamila.

Aidha DC Jamila ametoa Rai kwa Viongozi wote wa Dini ,Vyama vya Siasa pamoja na Waandishi wa Habari kuhakikisha kuwa wanaendelea kuhubiri umuhimu wa Amani ndani ya wilaya ya Mpanda na Taifa zima kwa ujumla huku akitolea mfano jinsi Baba wa taifa hayati Mwl.Nyerere alivyojenga Taifa la Tanzania kwa misingi ya Amani na Mshikamano.

Kwa upande wao viongozi wa dini wamempongeza na kumshukuru Mhe.Jamila Mkuu wa wilaya ya Mpanda na kamati yote ya Usalama ya Wilaya ya Mpanda kwa kazi nzuri ya kulinda Amani waliyo ifanya kabla wakati na baada ya uchaguzi kwani juhudi zao ndiyo zimefanya mpaka leo hii watu wote watembee kifua mbele huku wakiwa na Amani tele pasipo kuwa na uharibifu wa aina yoyote wa Mali ya Umma wala upotevu wa nguvu kazi ya Taifa

“Nikushukuru sana Mhe.mkuu wa wilaya kwa kazi nzuri uliyoifanya pamoja na wajumbe wote wa kikao hiki kwa kazi nzuri ambayo mmeifanya kabla wakati na baada ya uchaguzi,kazi ile mliyoifanya ndiyo imetufanya hapa leo tutembee kifua mbele huku tukiutaja mkoa wetu kwamba uchaguzi umekwenda salama na mkoa umebaki salama,hii yote ni matunda ya kazi nzuri ambayo tumeifanya” Amesema Mchungaji wa Kanisa la Moravian Mpanda Mjini.

Kamati ya amani na maridhino Wilaya ya Mpanda inaudwa na Viongozi wa Dini,vyombo vya ulinzi na usalama na viongozi wa vyama vya siasa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages