WAFANYAKAZI WA MANISPAA MPANDA HATARINI KUPATA MAGONJWA YA KUAMBUKIZWA

 

Wafanyakazi wanaofanya kazi ya kupakia taka ngumu katika maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Mpanda wakiwa wanapakia taka  ngumu kwenye Roli la  Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda lenye Namba za usajiri SM 12244 ambao wapo hatarini kupatwa na  magonjwa mbali mbali kutokana na kufanya kazi hiyo  pasipokuwa na vifaa vya kujinga kuambukizwa maradhi

Na Walter Mguchuma,Mpanda.

Wafanyakazi wa Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi wanaofanya kazi ya kupakia taka  ngumu  kwenye  Maeneo mbambambali ya  Halmashauri ya Manispaa Mkoa wa Katavi wapo hatarini  kupatwa na magonjwa mbambali ya kuambukiza kutokana na kufanya kazi hiyo pasipo kuwa na  vifaa vya kujikinga kama vile Maski.

Kama unavyoona kwenye picha hao ni wafanyakazi wa kuokota taka ngumu wakiendelea na kazi yao,Lakini hawana mavazi yoyote ya kujinda na afya zao.


Wafanyakazi wanaofanya kazi ya kupakia taka  ngumu  kwenye  Maeneo mbambambali ya  Halmashauri ya Manispaa Mkoa wa Katavi wapo hatarini  kupatwa na magonjwa mbambali ya kuambukiza kutokana na kufanya kazi hiyo pasipo kuwa na  vifaa vya kujikinga kama vile Maski.

Wakiongea na mwandishi wa Habari wakati wakiwa wanaendelea  kufanya shughuli hiyo leo hii  kwenye Maeneo ya Manispaa hiyo wamedai kuwa kilio cha wao kukosa vifaa kimekuwa  cha muda mrefu  sasa  na swala hilo wamesha lifikisha  kwa uongozi wa Manispaa hiyo lakini hakuna jitihada ambazo zimefanyika hadi sasa .

Mmoja wa wafanyakazi hao jina tunalo aliyekuwa akipakia taka nguvu kwenye Roli  la Manispaa hiyo lenye Namba za usajiri  SM 12244  ameeleza kuwa  wapo hatarini kupata  magonjwa ya kuambukiza  kutokana na shughuli wanayofanya ya kupakia taka wakiwa hawana vifaa wanavyopaswa kuwa navyo  vya kujikinga ili wasiweze kupata  maladhi mbambali .

Amebainisha kuwa  licha ya wao kuomba wapatiwe vifaa vya kujikingia kwa muda mrefu sasa Manispaa imekuwa  haiwajali  hali ambayo  inawafanya kwa kiasi kikubwa kuwa  hatarini  kupats magonjwa.

"...kazi hii ni ngumu sana inahitaji umakini mkubwa wakati unaifanya,suala la kujilinda dhidi ya afya zetu linategemea sana vifaa maalumu vya kutetendea kazi  hasa kuvaa...nashangaa kwa nini uongozi wa manispaa hawalitambui hilo nauliza ni nini kusudi lao?.Je ni kuona tunapata magonjwa?" amehoji kwa uchungu mmoja ya wafanyakazi hao.

Amefafanua kuwa  baadhi yao wenyeuwezo wameanza kujinunulia  viatu aina ya gun but ingawa kwenye kundi lao walioweza kununua viata hivyo hawazidi watatu .

Amesesema wanashangazwa  na  Halmashauri ya Manispaa  kuweza kushindwa kuwapatia hata maski ambazo  gharama zake ni ndogo mmno  hivyo wanaomba  waangalie uwezekano wa kupatiwa vifaa husika vya kufanyia kazi ili waepukane na hali ya sasa ya kuwa hatarini kupatwa na magonjwa yakiwepo ya mlipuko .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages