PASS TRUST YALETA NEEMA KATAVI


Watumishi wa Taasisi ya  PASS TRUST  mara baada ya kumalizika kwa kongamano la wadau wa kilimo wa Mkoa wa Katavi liliofanyika katika ukumbi wa Lyamba Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi . lililoandaliwa na taasisi hiyo na kuwashirikisha wadau wa sekta ya kilimo kutoka Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi

 

Na  Walter Mguluchuma.

    Katavi .

Taasisi ya  PASS TRUST ambayo   inayoshughulika  na kuwawezesha  wajasirimali wote ambao wapo kwenye  mnyororo wa kilimo  wamezindua kampeni ya  Kijanisha Maisha  katika Mkoa wa Katavi  ili kuunga juhudi za Serikali na Dunia kwa ujumla  katika swala zima  la  kutunza mazingira hasa kwenye  sekta  ya kilimo ambacho ni sehemu kubwa ya nchi   nchi na inayotowa  ajira na  kipato  katika  Nchi yetu ya Tanzania .


Baadhi ya washiriki wa kongamano la wadau wa sekta ya  kilimo katika  Mkoa wa Katavi walipokuwa kwenye kongamano la kilimo lililoandaliwa na PASS  TRUST liliofanyika katika ukumbi wa Lyamba Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi.


Taasisi ya  PASS TRUST ambayo   inayoshughulika  na kuwawezesha  wajasirimali wote ambao wapo kwenye  mnyororo wa kilimo  wamezindua kampeni ya  Kijanisha Maisha  katika Mkoa wa Katavi  ili kuunga juhudi za Serikali na Dunia kwa ujumla  katika swala zima  la  kutunza mazingira hasa kwenye  sekta  ya kilimo ambacho ni sehemu kubwa ya nchi   nchi na inayotowa  ajira na  kipato  katika  Nchi yetu ya Tanzania .

Uizinduzi huu katika Mkoa wa Katavi umezinduliwa katika  mkutano maalumu ambao uliwashilikisha wadau wa sekta ya kilimo uliofanyika katika ukumbi wa Lyamba katika Manispaa ya Mpanda na uliwashilikisha wadau wa kilimo kutoka katika Halmashauri zote tano za Mkoa wa Katavi

Mwakilishi  wa Mkurugenzi Mtendaji  wa  Pass Trust  Hermani Bashiri ambae ni meneja wa  maendeleo ya biashara amesema kuwa uzinduzi uliofanyika Mkoani Katavi ni mwendelezo tuu wakampeni ambayo imeisha zinduliwa tayari  hivyo  aliwahakikishia  wanafika kwenye kila Mkoa na kwenye kila Wilaya hapa Nchini  ili wadau wao wote waweze kupata taarifa na kuweza kuchukua furusa hii ya kijani shirikishi .

Amefafanua kuwa  Pass Trust ni asisi ya kusaidia  sekta binafsi ya kilimo  ni chombo ambacho kilianzishwa   mwaka 2000 ili kuchochea  uwekezaji  na kukuza  kilimo  cha biashara    na sekta zinazo husika katika mnyororo wa kilimo  .

 Amebainisha kuwa walengwa wakubwa kwenye mradi huu ni  wajasiriamali wote ambao wapo kwenye mnyororo wa  kilimo  kuanzia mtu binafsi mmoja mmoja  au kwa njia ya vikundi vilivyosajiriwa na Halmashauri na taasisi nyingine ambazo zinashughulika na kilimo na  mnyororo wake wa thamani ya kilimo .

Bashiri ameeleza kuwa  wanawajibika  katika utoaji wa  huduma  za maendeleo  ya kilimo  cha biashara  kwa ,wajasiriamali wadogo  na wakati  kwa kuwaunganisha  na taasisi za fedha ambao mpaka sasa wanafanya kazi na taasisi za kifedha Zaidi ya kumi nan nne  hapa nchini .

 Amesema kuwa  pia  malengo yao PASS   Trust ni kuchochea  uwekezaji  na kuhimiza ukuaji  wa kilimo    nchini Tanzania  na dira yao  ni kuwa asasi  inayoongoza  katika  utoaji  wa huduma za fedha  na maendeleo  ya biashara katika  sekta ya kilimo hapa nchini .

Kuhusu huduma za fedha  watawasaidia  watu  na makampuni  wanaositahili kupata   mkopo  kwa ajiri ya uwekezaji  wenye  faida  kupitia tathimini ya maandiko  ya kuwaombea  mikopo kulingana  na benki husika .

Amesema kipaumbele kitatolewa kwawatejawenye  matokeo  makubwa  katika  mwendelezo  wa mnyororo  wa  thamani  wa bidhaa za kilimo  husani  katika mazao ya chakula ,biashara  na mazao ya kusafirishwa nje .

Nae  Neema Zakaria  mmoja wa wadau wa sekta ya kilimo  ameshukuru  kwa taasisi hiyo kwa kuweza kufika   Mkoani  Katavi na kufanya kongamano ambalo  limeambatana na mafunzo  ambayo yamekuwa tija kubwa sana kwao  kwa ajiri ya kufanya biashara zao za mnyororo wa kilimo ..

Edward  Mlanda  amewashukuru PASS  kwa furusa waliowaletea ambayo hawakuwa nayo wao hasa wakulima wengi walikuwa wanashindwa kuchukua mikopo  kulingana na mazingira  lakini sasa   kwa udhamini wa PASS Sasa  watanufaika .

Amewaomba wakulima wenzake wa Mkoa wa Katavi wasiogope kuchukua  mikopo   kwa kutokuwa na mdhamana  kwani  sasa   mdhamini PASS wameisha  jitokeza  bila kujari  wametokea kwenye mazingira gani huo  kwao ni msaada  mkubwa sana kwa wakulima

 Afisa kilimo wa Mkoa wa Katavi Faridu Abdalla  amesema kuwa kuna changamoto mbali mbali amzazo zimekuwa zikiwakabili vijana wa Mkoa wa Katavi kwenye sekta ya kilimo miongoni mwa changamoto  hiyo ni  vijana wengi  kutokuwa na umiliki wa ardhi .

 Pia vijana wengi  wamekuwa na mtazamo hasi kwenye kilimo  kwa kudhani kuwa shughuli ya kilimo hufanywa na wazee tuu jambo ambalo sio la kweli .

Changamoto nyingine ameeitaja kuwa ni  vijana kutotambua  furusa  za uhuhimu wa kilimo  na pia wamekuwa  wakishindwa kuumudu gharama za uwendeshaji wa shughuli za kilimo kutokana nakuwa na uwezo mdogo wa kiuchumi .

Amesema kuwa  Mkoa wa Katavi bado hauja tumia furusa inavyotakiwa kwenye sekta ya kilimo kwani  kuna ekari laki tisa ambazo zinafaa kutumika kwa shughuli za kilimo lakini kati ya ekari hizo ni ekari laki mbili na nusu tuu ndio zinazotumika kwa shughuli za kilimo  kwenye Mkoa huu.

Mwakilishi wa   Mkuu wa Mkoa wa Katavi Neemia James  Katibu  Tawala  msaidizi Uchumi na   Uzalishaji  wa  Mkoa wa Katavi amewataka wananchi wa Mkoa wa Katavi kutumia  furusa ya uwepo wa PASS katika kuboresha shughuli zao za kilimo na usindikaji wa mazao yao mbambali watakayo kuwa wanazalisha .

Kubwa  Zaidi ni swala la mikopo taasisi hiyo inawasaidia wakulima  na wasindikaji wa mazao mbali mbali kwenye kuboresha kilimo  chao na   shughuli za usindikaji hali ambayo itawafanya waongeze pato lao na kufanya shughuli zao za kilimo kwa uhakika mkubwa .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages