MWENGE WA UHURU MPANDA KUZINDUA MIRADI YA ZAIDI YA BILIONI 2

 

Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph akitoa taarifa ya Maandalizi ya Mapokezi ya Mwenge wa Uhuru kwa Viongozi mbalimbali wa Wilaya ya Mpanda katika kikao cha Tathimini ya Mwisho kwaajili ya kuupokea mwenge wa uhuru 


Na Paul Mathias,Mpanda

Wananchi katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameobwa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru unaotalajia kuanza Kukimbizwa Wilaya ya Mpanda Mnamo 25 /8/2023.


Wananchi katika Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi wameobwa kujitokeza kwa wingi kuulaki Mwenge wa Uhuru unaotalajia kuanza Kukimbizwa Wilaya ya Mpanda Mnamo 25 /8/2023.

Akitoa taarifa ya maandalizi ya kuelekea kuupokea Mwenge huo katika kikao kazi kilicho fanyika Ukumbi wa Mikutano wa Manispaa ya Mpanda Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Jamila Yusuph amesema Mwenge wa Uhuru unatalajia kukimbizwa katika Halmashauri zote mbili za Wilaya ya Mpanda, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Halmshauri ya Nsimbo.

Mwenge huo wa Uhuru unatalajia kukibizwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda 25/8/203 na 26/8/2023 Katika halmashauri ya Nsimbo Wilaya ya Mpanda.

Jamila yusuph amesema kuwa Mwenge huo utazindua,Kuweka Mawe ya Msingi na kutembelea Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika Wilaya ya Mpanda yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 2 na Milioni 671 na laki tatu na Sitini .

Amesema katika Manispaa ya Mpanda Miradi yenye Thamani ya Shilingi Bilioni 1 na Milioni 774 huku Halmashauri ya Nsimbo miradi itakayofikiwa na Mwennge wa Uhuru itakuwa na Thamani ya Shilingi Milioni 897 na 52 Elfu .

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Wilaya amesema Mwenge wa uhuru utazindua miradi mbalilmbali ya Maenndeleo katika Wilaya ya Mpanda.

‘’tunavyo vyumba viwili vya Madarasa kule halmashauri ya Nsimbo vyenye Thamani ya Shilingi Milioni 40 upo mradi wa Maji Kapanda wenye thamani ya Shilingi Milioni 265 laki mbili na arobaini na Saba,Zahanati ya Matandalani kule stalike yenye thamani ya Shilingi  Milioni 60,Vyumba vitano vya Madarasa shule ya Msingi Misunkumilo yenye thamani ya Shilingi Milioni 130 ‘’amesema Jamila yusuph Mkuu wa Wilaya ya Mpanda.

Ameitaja miradi mingine itakayozinduliwa na Mwenge huo kuwa ni pamoja na ‘’Mradi wa Maji kakese wenye thamani ya Shilingi Milioni 950,Daraja la Kashaulili lenye Thamani ya shilingi Milioni 160 na lakimbili na arobaini na saba hii ndiyo miradi itakayo zinduliwa na Mwenge wa Uhuru kwa Wilaya ya Mpanda  ‘’amesema Jamila Yusuph  mkuu wa Wilaya ya Mpanda.

Pamoja na hayo ameeleza kuwa miradi mbalimbali itawekewa Mawe ya Msingi na Mwenge huo wa Uhuru miradi hiyo nipamoja na Ujenzi wa Barabara ya Lami Mita 745 halmashauri ya Nsimbo yenye thamani ya shilingi milioni 494 na elfu sabini na Tisa na mianane,Shule ya Mchepuo wa kiingereza yenye Thamani ya Shilingi Milioni 160 ,Kituo cha Afya Kazima Jengo la OPD,Maabara na Jengo la kichoma taka vyenye thamani ya Shilingi Milioni 250.

Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2023 Ubeba Kaulimbiu isemayo Tunza Mazingira okoa vyanzo vya Maji kwa usitawi wa Viumbe hai na Taifa kwa Ujumla.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages