Na Paul Mathias, Katavi
Benki ya CRDB Tawi
la Mpanda Mkoa wa Katavi imetoa Madawati 162 kwa Shule Tatu za sekondari ili
kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa za serikali katika kuimarisha
miundo mbinu ya Elimu katika mkoa wa Katavi na Tanzaniakwa ujumla.
![]() |
Wanafunzi wa Sekondari Kawalyowa wakiwa wameketi kwenye Madawati yaliyotolewa na Benki ya CRDB Shuleni Hapo. |
Akikabidhi
Madawati hayo Katika shule ya Sekondari Kawalyowa na Maluja Sekondari zilizopo
Manispaa ya Mpanda pamoja na Sekondari ya Majalila iliyopo Wilaya ya Tanganyika
Meneja wa Benki ya CRDB Hamad Masoud amesema Benki hiyo inatoa msaada huo ikiwa
ni sehemu ya kurejesha wanachokipata kupitia wateja wao.
‘’Benki yetu ya
CRDB katika jitihada zake za kusaidia sekta ya Elimu Katika Mkoa wa Katavi tumetoa
msaada wa Madawati 162 Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya
Tanganyika na tutakwenda Hadi Halmashauri ya Mpibwe madawati haya kwa ujumla
wake yanathamani zaidi ya Shilingi
Milioni 7 ‘’amesema Masoud
![]() |
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Mpanda Hamad Masoud akimkabidhi Madawati Diwani wa Kata ya Kakese Maganga Salaganda katika Shule ya Sekondari Maluja iliyopo Kata ya Kakese. |
Kwa upande Emanueli
Biganio Afisa mahusiano Biashara na serikali kutoka CRDB Benki kanda ya Mbeya amesema
Benki hiyo imekuja na Kampeni maalumu inayojulikana kama Keti Jifunze ambao
utatekelezwa ambao utatekelezwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.
‘’Juhudi hizi za
kuunga mkono Elimu tunaufanya nchi nzima sio tu hapa Katavi ila nchi nzima mpango
huu tumeupa jina la Keti Jifunze tunataka watoto wakae na wasome kama vile
ambayo Serikali inasisitiza na kuendelea Kuboresha Miundo mbinu ya Elimu’’
amesema Biganio.
![]() |
Muonekano wa Shule ya Sekondari Maluja iliyopo Kata ya Kakese Manispaa ya Mpanda ambayo imepatiwa Madawati Kutoka Benki ya CRDB Benki |
‘’niwapongeze
CRDB kwa Msaada huu sisi wasimamizi wa Elimu tunaimani hiki walichokitoa
kitawasaidia wanafunzi hawa kukaa na kusoma kwa utulivu amesema’’ Kimeme
Salome antony
Mwanafunzi wa Sekondari Kawalyowa ameishukuru Benki ya CRDB Benki kwa kuwaletea
Madawati hayo watayatumia vizuri katika kujifunza na kuongeza maarifa katika
kutimiza ndoto zao kielimu.
![]() |
Meneja wa CRDB Benki Tawi la Mpanda Hamad Masoud akimkabidhi Dawati Mkuu wa Shule ya Sekondari Majalila |