ZAIDI YA WANANCHI 800 KATAVI WAPATIWA MATIBABU NA MADAKTARI BINGWA

Baadhi  ya wananchi waliojitokeza kupatiwa huduma   na  madaktari bingwa Bobezi wa kutoka katika Hospitali ya Rufaa ya Benjamini Mkapa wakiwa  katika  hospital ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi


Na Walter Mguluchuma,Katavi

zaidi ya Wananchi   1000 wamejitokeza kwa muda wa siku tano  kuweza  kupatiwa  matibabu mbalimbali yaliyotolewa  na   madakitari  Bingwa wabobezi wa  kutoka Hospitali ya Rufaa ya Benjamini  Mkapa huku mwikio wa wananchi waliofika kupatiwa huduma hizo ukiwa ni mkubwa

Mkuu wa  Kitengo cha     mawasiliano na  mahusiano wa  Hospitali ya  Rufaa ya  Benjamini Mkapa  Jeremia  Mbwambo  akielezea   namna ambavyo  madakitari   bingwa   bobezi  wa  Hospitali ya  Benjamini  Mkapa walivyoweza kufanya kazi za kuwahudumia wananchi   mpaka  muda usiku wa  manane pasipo  kuchoka

 

zaidi ya Wananchi  1000 wamejitokeza kwa muda wa siku tano  kuweza  kupatiwa  matibabu mbalimbali yaliyotolewa  na   madakitari  Bingwa wabobezi wa  kutoka Hospitali ya Rufaa ya Benjamini  Mkapa huku mwikio wa wananchi waliofika kupatiwa huduma hizo ukiwa ni mkubwa

Daktari Kiongozi  anae husika na usimamizi wa utowaji wa huduma bora katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt  Parason  Mtasingwa alisema wamepokea  madakitari Bingwa  wabobezi   12 kutoka katika Hospitali ya Rufaa ya Benjamini  Mkapa  toka  tarehe 11  mwezi huu hadi  tarehe  15 mwezi huu walipohitimisha  utowaji wa huduma hizo  wakiwa wameshirikiana na madaktari wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi .

Mwitikio wa wananchi umekuwa ni mkubwa   kwa sababu wako juu sana malengo ya wagonjwa  waliokuwa wamepanga kuwahudumia kwa muda  huo wa siku tano  kwani  kwa muda wa siku  nne walikuwa wamewaisha wahudumia wagonjwa  879 ambao  wako zaidi ya wagonjwa waliokuwa wamepanga kuwahudumia kwa muda wa siku tano .

Mbunge wa Viti   maalumu  Mkoa wa Katavi Tasca  Mbogo  akielezea  namna  alivyopata wazo la kuwaomba  madaktari  Bingwa   bobezi wa Hospitali ya Benjamini Mkapa kuja   mkoani Katavi kutowa huduma za   udaktari bingwa baada ya kuona kuna mahitaji hayo na amewahakikishia wananchi     atawaomba waje tena kutona na jinsi watu  wanavyohitaji  kuduma hiyo

Sambamba  na hilo wapo zaidi ya wagonjwa   zaidi ya mia mbili ambao wameweza kufika lakini hawakuweza kuwahudumia  kutokana mwitikio huo wa watu kuwa mkubwa  wagonjwa kuwa wengi na ufupi wa muda wa siku za   zilizipangwa kutowa huduma .

Alisema  kwa ujumla zoezi hilo limekwenda  vizuri kwa watuwalipatiwa huduma  kwani  wagonjwa waliofika wameweza kapatiwa huduma za  vipimo   upasuaji  ,dawa na ushauri  kuhusu afya zao na  kwa   wagonjwa walionekana na matatizo  makubwa   hasa ya upasuaji  umewekwa utaratibu  mzuri wa kuweza kuwafuata  huko huko  madakitari   bingwa hao ili wakaweze kufanyiwa upasuaji  mkubwa katika Hospitali ya Benjamini  Mkapa .

Dkt Mtasingwa amemshukuru   Rais  Dakta   Samia  Suluhu Hassani  na Wizara ya  Afya  kwa kuweza kuwajengea uwezo wa  udaktari   Bingwa na ubobezi kwa     hao  madaktari  na pia kuweza   kuziwezesha  taasisi mbalimbali  zinazotowa huduma  kwa upande wa afya .

Amebainisha kuwa   kwa  muda huo wa siku tano madakitari bingwa   wabobezi hao wameweza  kufanya  opesheni 49 za magonjwa mbalimbali  na  bado walikuwa wakiendelea na   upasuaji mwingine kwenye siku        ya tano ya kumalizia kutowa huduma kwenye Hospitali hiyo ya Katavi .

Alifafanua kuwa idara ya magonjwa  ya akina mama  na  uzazi . watoto  mifupa  na magonjwa ya ndani  yamekuwa na mwitikio  mkubwa sana wa magonjwa  pia wamemshukuru  Mbunge wa Viti Maalumu   Tasca   Mbogo  kwani  amekuwa karibu sana na madaktari hao kwa muda wa siku  zote tano amekuwa akiwapa ushirikiano mkubwa  katika kuhakikisha huduma zinatolewa kwa wananchi  kwa jinsi ilivyokusudiwa .

Mbunge wa Viti Maalumu  Mkoa wa Katavi Tasca Mbogo  amesema watu wamejitokeza kwawingi kwani ukiangalia jiografia ya Mkoa wa Katavi mtu anapokuwa amepewa rufaa ya  kwenda Hospitali ya  Kanda kwa ajiri ya kupatiwa matibabu   ulazimika kusafiri  umbali wa kilometa  mia  nane hivyo ndio maana wamejitokeza kwa wingi kutokana na huduma hiyo ya kibingwa kusogezwa karibu .

 Mbogo alieleza kuwa kutokana na mahitaji ya watu wa Mkoa wa Katavi  kuhitaji  huduma za  madaktari bingwa bobezi ndio maana yeye  alipata wazo  la kuomba   Madaktari   bingwa  bobezi kutoka katika  hospitali ya  Benjamini  Mkapa waweze kufika katika hospitali ya Mkoa wa Katavi .

 Kwanza  alimshukuru  Rais  Dkt  Samia kwa kujali   afya za Watanzania  na kwa  ujenzi wa Hospitali za Rufaa za  mikoa na vituo vya afya  katika ujenzi huo mafanikio hayo yameweza kusaidia  mkoa wa  Katavi  kwa kuweza kuwa na hospitali  ya Mkoa yenye madaktari bingwa na vifaa vya kutosha na ndio maana  madaktari  wa  Benjamini  Mkapa wameweza kufanya kazi bila  shida  kwani wamekuta kuna vifaa vya  kutosha na  vya kisasa .

Alisema kutokana na hali ya mwitikio kuwa  mkubwa amewaomba   madaktari bingwa wa  Benjamini Mkapa wasimchoke kwani  atawaomba tena kama alivyowaomba  wakati huu  waje tena  Mkoani  Katavi kuwahudumia  wananchi kwa kuwapatia matibabu na ushauri  kwani imeshindikana kuwahudumia wananchi wote  waliotijaji kutokana mwitikio kuwa  mkubwa na muda kuwa  mchache .

Taska  Mbogo  amewahakikishia wananchi wa  Mkoa wa Katavi  kuwa  ajitahidi  kadri ya  uwezo wake  madakitari hao  warudi tena katika Mkoa wa Katavi  ili waweze  kutowa tena huduma hiyo kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi

Nae Jeremia  Mbwambo  mkuu wa kitengo cha  mawasiliano  na  mahusiano wa   hospitali ya  Benjamini  Mkapa   alisema  lengo la  madaktari wa hospitali hiyo ilikuwa ni kuhudumia watu 400 hado 500  wameweza kufika watu zaidi ya 1000 waliohudumiwa ni 879 hivyo wamelazimika kutowa huduma wakati mwingine hadi usiku wa manane  hasa  kwenye  kufanya upasuaji .

Hali hiyo inaonyesha jinsi wadakitari hao walivyoamua kufanya kazi za  dhati za kuwahudumia wananchi wa Mkoa wa Katavi  na  pia imeonyesha jinsi  Mbunge wa viti Maalumu Tasca  Mbogo alivyowapokea   tangia alivyoanza kuratibu zoezi hilo toka mwanzo .

Mwambambo  amebainisha kuwa sio jambo dogo  kuleta  madakitari 12 waliokuwa wameongozwa na  Mkurugenzi wao Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa  maana unapowatowa kwenye hospitali ya rufaa unaona kuna mzigo  Fulani wa wananchi utakuwa umetoka katika kuwahudumia wananchi  lakini kutokana na jinsi walivyojipanga ndio maana walikubali  madakitari hao waweze kufika Katavi  ni jambo la kumshukuru  Mkurugenzi wao  Dkt  Alfonce   Chandika  kwa kuweza kuridhia 

Mkazi wa  Mtaa wa Mtaa wa Makanyagio  Manispaa ya Mpanda Crekensia  Malango  aliwashukuru  Madakitari  kwa kuweza  kumfanyia upasuaji mkubwa  mtoto wake  aliyekuwa  anatatizo la kuwa na  utumbo mkubwa lakini baada ya kufanyiwa upasuaji huo  mwanae kwa sasa anaendelea vizuri huku akiwa bado anapatiwa matibabu  .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages