MADAKTARI BINGWA WA BENJAMINI MKAPA WATOWA HUDUMA YA MATIBABU KATAVI APIGA KAMBI KATAVI

Mkurugenzi Mtendaji wa Hosptali ya Benjamin Mkapa-Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi.

Na  Walter   Mguluchuma,Katavi.

Madaktari   Bingwa wabobezi wa  Hosipitali ya Rufaa ya Benjamini   Mkapa  wameanza kutowa huduma ya matibabu ya udaktari wa kingwa  wa magonjwa      mbalimbali  ikiwa ni  jitihada  za  Hospitali hiyo kuwafikishia  Wanzania huduma za kiafya mahali walipo,

Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mwanamvua Mrindoko wakati akizungumza na madaktari bingwa na bingwa bobezi (Hawaonekani kwenye picha) katika ofisi yake leo.

Mkurugenzi wa  Hospitali ya  Benjamini  Dkt  Alphoce  Chandika  ambae  ameongoza timu hiyo ya     madaktari   amebainisha kuwa wapo  Mkoani   Katavi kwa ajiri ya kutowa huduma za kiafya  kwa kuwa moja ya  adhima ya Serikali  imeisha towa  mwongozo  unao wataka watoke nje ya Hospitali na kwenda kuwahudumia wananchi huko waliko na ndio maana wameamua kufika  Katavi .

Mkoa wa Katavi ni   moja wapo wa maeneo ambayo yamekuwa yakituma wagonjwa mbalimbali kwenda kutibiwa   katika Hospitali ya Rufaa ya Benjamini Mkapa  kama sehemu yao ya  rufaa kwa kuwa  Hospitali hiyo ni  moja  katika ya Hospitali za  Rufaa za Kanda  zinazotowa huduma za kibingwa hapa  nchini .

Dkt Chandika  ameeleza kuwa wamekuwa     kwenye  Hosipali ya  Benjamini  Mkapa  wakiwa  na wataalamu  waliopata  ujuzi wa  kidaktari ndani na je ya nchi  kwa ajiri ya kuwahudumia wananchi  na  wameanza kutowa huduma za ubingwa  bobezi  ukiwemo  upandikizaji wa figo  na kuna maabara  maalumu   kwa ajiri ya magonjwa ya moyo  kwa mantiki hiyo  hizi huduma zinatakiwa kuwafikia wananchi  hivyo wameamua kufika Katavi  ili kuwahudumia wananchi  pasipo wao  kusafiri umbali  mrefu  kwenda Dodoma.



Baadhi ya Madaktari bingwa na bingwa bobezi kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma wakishuka kwenye ngazi baada ya kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Amefafanua kuwa wamekuwa wakipata wagonjwa wengi kutoka kwenye ukanda  huu kwani  levo ya  Hosiptali ya  Mkoa wa  Katavi sio  huduma zote za matibabu ya  kidaktari bingwa  zinaweza kuwa zinapatikana  hivyo   Serikali ya   awamu ya sita  imewawezesha vifaa vya kuweza kutowa huduma hiyo ya  mkoba  na ndio maana   waweza kufika  Katavi  kwa kuwa patia wananchi  huduma zilizoimarika  mahali wanapo ishi .

Wapo   Mkoani  Katavi      madaktari 12  wa kutoka   Benjamini  Mkapa  ambapo watajikita zaidi  kwenye utaalamu wa  magonjwa kumi na moja  ambapo wanae  daktari bingwa wa  magonjwa ya ubongo na mishipa ya  fahamu kwani wamebaini  kuna watotowanaotoka  huku kwenda kutibiwa huko  wanaozaliwa wakiwa na vichwa vikubwa  hivyo wamekuja na vifaa ambavyo watawahudumia hapo hapo kwenye  hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Katavi na kuwapunguzia adha ya usafiri .

Pia wanae  dkt wa  magonjwa wa  mfumo wa  mkojo  kwa kuwa tatizo hilo lipo kwa wazee,wanae pia  dkt wa watoto  wamebaini kuna   matatizo ya watoto wanaozaliwa wakiwa na matatizo ya  moyo  vilevile wanamadaktari bingwa wa   mifupa na viungo .

Amewataja  madaktari wengine kuwa ni  wamagonjwa ya kina mama na  uzazi  macho   figo  wanawashukuru  Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa wa Katavi  na  Mikoa ya jirani  wajitokeze kwa wingi kwani wao wamejipanga kuwahudumia wote pia mbali ya kutowa matibabu watatowa  pia na ushauri kwa watu wenye magonjwa mbalimbali .

Mkuu wa  Mkoa wa Katavi  Mwanamvua  Mrindoko   ametowa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Katavi kujitokeza  kwa wingi  kuweza kupatiwa huduma za  madakitari bingwa hao kwani  haja wahi kupokea  malalamiko yoyoye ya kutoka kwa wananchi  wanaokuwa wanakwenda kutibiwa katika Hospitali ya Benjamini  Mkapa hali hiyo inaonyesha jinsi huduma zao zilizokuwa na   ubora .

Amesema kuwa ni vema wananchi watumie furusa hiyo  ambayo itakayokuwa inatolewa  ili  waweze kupatiwa huduma  nzuri  pamoja na ushauri  anafahamu  Mkoa wa Katavi unayo  hospitali ya   Mkoa ya  Rufaa  lakini  haina   madakitari bingwa  lakini  bado  hawaja timiza  madakitari bingwa wa kwenye vitengo vyote .


Kaimu  Mganga   Mfawidhi wa Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt  Damiani  Maruba   ameeleza kuwa ujio wa    wataalamu


Kaimu  Mganga   Mfawidhi wa Hospitali ya  Rufaa ya Mkoa wa Katavi Dkt  Damiani  Maruba   ameelez

a kuwa ujio wa    wataalamu   utawasaidi  wao  kuweza kujiongezea  utaalamu zaidi ambao hawakuwa nao   awali .

Aidha   amesema    hospitali hiyo    haina wataalamu  mbalimbali kama vile  wa   watoto ,figo   magonjwa ya ndani , mtaalamu wa  magonjwa ya ufahamu   mtaalamu  mbobezi wa mfumo wa chakula  hizo ni  baadhi ambazo    hawana wataalamu kwenye Hospitali ya Rufaa ya  Mkoa wa Katavi.

Dkt Maruba  amesema    kwa      timu hiyo ya  madakitari inatarajiwa kufanya kazi katika Mkoa wa Katavi kwa  muda wa siku  tano ambao kwa siku ya kwanza wameweza kujitokeza watu zaidi ya  150

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages