RUWASA KUJA NA MFUMO WA KIMTANDAO KUTHIBITI UPOTEVU WA MAPATO JUMUIYA ZA WATUMIA MAJI VIJIJINI

Mwenekiti wa Halmashauri ya Nsimbo Charles Halawa akizungumnza na wajumbe wa kikao cha baraza la Madiwani Halmashauri ya Nsimbo.

 Na Paul Mathias,Nsimbo

Baraza la madiwani katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi mkoa wa Katavi wameishauri Wakala wa Maji na usafi wa Mazingira Vijijini [RUWASA]  kuwa  na utaratibu wa kuthibiti Mapato yanayokusanywa na jumuiya za watumia maji vijijini ili kuendeleza miradi mingine.

Madiwani katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi wakiwa katika Kikao cha Baraza la Madiwani

Baraza la madiwani katika Halmashauri ya Nsimbo Mkoa wa Katavi mkoa wa Katavi wameishauri Wakala wa Maji na usafi wa Mazingira Vijijini [RUWASA]  kuwa  na utaratibu wa kuthibiti Mapato yanayokusanywa na jumuiya za watumia maji vijijini ili kuendeleza miradi mingine.

Hoja hiyo imebuliwa na Madiwani hao katika Kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kinajadili taarifa za taasisi naza Kata kwenye Halmashauri hiyo.

Akichangia hoja ya taarifa ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Wilaya ya Mpanda  Diwani wa kata ya Machimboni Raphael Kalinga amesema kuwa jumuiya za watuamiaji katika kata yake imekuwa ikikusanya mapato mengi ila changamoto ya Matumizi ya fedha hizo imekuwa na ukakasi.

Meneja wa Ruwasa Wilaya ya Mpanda Mhandisi Christian Mpena akitoa taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya Maji Halmashauri ya Nsimbo kwenye kikao cha Baraza la Madiwani

Kalinga anasema ‘’chombo hiki kwenye Kata yangu kimekosa hata akiba mfano kama kule kwangu wanakusanya hadi Milioni 11 ukijakuangalia akiba Milioni mbili tunafahamu kuwa malengo ya chombo hiki kukusanya fedha ili iendeleze miradi mingine’’ anasema Kalinga.

Amesema kuwa jumuiya hizo zikisimamiwa vizuri katika ukusanyaji wa Mapato utaisadia serikali kupata mapato na kujiendesha kwa vyombo hivyo Vijijini.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mtapenda Elieza Fyula ameishukuru Ruwasa kwa kundelea kutekekeleza miradi Maji vijijini na kuwaomba Ruwasa kuendelea kusambaza Maji katika maeneo ya Taasisi mpya za serikali ili wananchi waendelee kupata huduma bila usumbufu.

‘’Shule mbalimbali zinazoanshwa kwenye Halmashauri yetu ikiwemo shule ya Msingi Shelesi na shule mbalimbali zilizoanzishwa niwaombe Ruwasa muangalie Bajeti muone uwezekano wa kuchimba visima vya maji ili wanafunzi na walimu waliopo katika taasisi hizo waweze kutumia maji hayo’’ amesema Fyula

Kwa upande wake Michael Kasanga Diwani wa Kata ya Nsimbo ameiomba Ruwasa kuangalia uwekezakano wa Maji yanayotumika katika kijiji cha Mwenge kusaidia kuyafikisha Kijiji cha Kanoge nambamoja na Filimule ili wananchi wa Maeneo hayo wapate huduma ya Maji.

Christian Mpena Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mpanda akiwasailisha taarifayake kwenye Baraza hilo amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2023/2024 Ruwasa katika halmashauri ya Nsimbo itakwenda kujenga mradi wa Maji katika kijiji cha Kabuga na Bulembo wenye Ghara ya zaidi ya Bilioni moja .

Mpena amesema kuwa watakwenda kutekeleza mradi wa kubadilisha Pampu za mkono kwenye kwenye visima kijiji cha masewela,Filimule' Kabulonge, Kapunga, Katumba ,Kapalala na kijijji cha Kabatini.

Kuhusu uthibiti wa Mapato kwenye jumuiya za watumiamaji Mpena Amesema kuwa Serikali siku chache zijazo inakuja na mfumo wa kulipia maji kwanjia ya Mtandao hali ambayo itasaidia kupunguza ufujaji wa pesa zinazotokana tozo za maji kwa wananchi

‘’Ripoti ya CAG inaonesha kuna baadhi ya Vyombo wametumia Pesa Mbichi kwa hiyo serikali inakuja na mfumo mpya wa Makusanyo ya fedha kwa njia ya mtandao BLT watalamu wa B.OT wanakuja wiki ijayo kwaajili ya mafunzo ya GEPG kwahiyo wananchi wote watakuwa wanalipia maji kwa njia ya Control Number ukilipa kwa Control namba fedha inaingia moja kwa moja Benki kuu anasema Mpena ‘

Mohamed Ramadhani Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Nsimbo ameomba Mfumo wa kununua maji kwa njia ya Luku ufungwe kwenye taasisi za serikali ili kuepusha malimbikizo ya Bili za maji ambazo zimekuwa zinajitokeza kwenye taasisi hizo.

Charles halawa mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo ameipongeza Ruwasa kwa kuendelea kutekeleza miradi ya Maji kwenye maeneo mbalimbali ya Halmashauri hiyo ili wananchi hususani akina mama waondokane kutumia muda mwingi kutafuta maji.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages