CBWOSS 22 KATAVI ZAPIGWA MSASA MFUMO WA MALIPO YA SERIKALI GPG

Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Katavi Mhandisi Peter Ngunula akifunga Mafunzo kwa watoa huduma ngazi ya jamii CBWOSS zipatazo 22 katika mkoa wa Katavi yaliyodumu kwa muda wa siku 10

 
Na Paul Mathias-Katavi

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Mkoa wa Katavi inatalajia kuongeza ukusanyaji wa Mapato kupitia huduma ya utoaji wa Maji vujijini baada ya kuanza kutumia Mpya wa malipo ya Huduma ya Maji kwanjia mtandao uliounganishwa na Mfumo wa Malipo ya Serikali GPG.

Watoa huduma ngazi ya jamii CBWOSS Katika mkoa wa Katavi wakila kaipo cha utii kwa kazi watakazoenda kuzifanya baada ya kumaliza kupatiwa semina ya kufanya kazi na mfumo wa Malipo ya serikali katika kazi zao.

Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini Ruwasa Mkoa wa Katavi inatalajia kuongeza ukusanyaji wa Mapato kupitia huduma ya utoaji wa Maji vujijini baada ya kuanza kutumia Mpya wa malipo ya Huduma ya Maji kwanjia mtandao uliounganishwa na Mfumo wa Malipo ya Serikali GPG.

Akizungimnza wakati akifunga Semina ya Siku kumi kwa viongozi wa utoaji wa huduma ya Maji ngazi jamii CBWOSS Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Katavi Mhandisi Peter Ngunula amesema kuwa mfumo huo utasaidia katika ukusanyaji mapato kwakuwa wateja watalipia bili zao za huduma ya Maji kwa njia ya simu na fedha hizo kuingia katika mfumo wa malipo ya serikali.

Ngunula amesema kuwa Ruwasa Mkoa wa Katavi itaendelea kutoahuduma ya Maji Vijijini kwa kadri inavyowezekana ili wananchi waendelee kupata huduma ya Maji kwa ukaribu Zaidi kwa kuweka miundombinu rafiki kwenye makazi yao.

Washiriki wa Mafunzo hayo wakimsikiliza kwa umakini Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Katavi Mhandisi Peter Ngunula akifunga mafunzo hayo.

Amewaasa Viongozi wa utoaji huduma ya Maji ngazi ya Jamii kwenda kufanya kazi kwa kuzingatia weledi na uzalendo kupitia mafunzo waliyoyapata kwa kuwahudumia wananchi pasipo na kikwazo chochote ikiwa ni sehemu ya kuiasaidia serikali katika kuongeza Mapato kupitia Ruwasa.

''JukumukubwalaMsingi ambalo mmelisema kwenye kiapo nikuhakikisha mnazingatia  maadili mmekula viapo lakini ni dhahili kwamba hatua kali zitachukuliwa kwa wale wote ambao watakwenda kinyume na viapo hivi msitumie fedha   mbichi akaunti za   makusanyo  zipo fedha  zote  zipelekwe Benki  amesema      Mhandisi ‘’Ngunula.

Kwa upande wake Masoud Almasi Kutoka Wizara ya Maji kitengo cha Tehama amesema kuwa katika Mkoa wa Katavi wameweza kuziingiza katika mfumo jumla ya CBWOSS 22 kutoka wilaya zote za Mkoa wa Katavi zikiwa na jumla ya wateja wapatao 5467.

Masoud Almasi kutoka wizara ya Maji kitengo cha Tehama akitoa neno kwa washiriki wa Semina hiyo.

Ameeleza kuwa tangu waanze kutoa mafunzo hayo kwa kuzingaunisha CBWOSS katika mfumo wa malipo ya serikali jumla katika mikoa Sita Hapa nchini jumla ya CBWOSS 183 zimefikiwa na kuuganishwa  katika Mfumo huo wa GPG  na kufanya jumla ya Wateja wapatao 1,40227 waliounganishwa na Mfumo huo nchinzima.

Amewaomba washiriki waliopatiwa Mafunzo hayo kwenda kuongeza nguvu katika kusajili wateja wapya kwa njia ya Mtandao watakao hitaji huduma ya Maji kwenye maeneo yao kwakuwa tayari wameshajengewa uwezo namna ya kuwasajili wateja hao wapya kwenye CBWOSS zao.

Beata Joseph mmoja wa Washiriki wa Mafunzo hayo amesema mkuwa wanatalajia kwenda kuongeza makusanyo kwenye CBWOSS zao kwakuwa wamepatiwa mafunzo hayo ya kuwahudumia wateja kwa njia ya Mtandao hususani katika kufanya malipo ya bili zao za Maji.

Jumla ya Mikoa Sita Hapa nchini zinazotoa huduma ya Maji Vijijini Ruwasa imeweza kuunganishwa na mfumo wa Malipo ya Serikali GPG ili kuthibiti upotevu wa Makusanyo wa Mapato hayo mikoa hiyo ni Kilimanjaro,Shinyanga, Mwanza, Katavi,Rukwa,Morogoro, na Mwanza. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages