Na Paul Mathias,Katavi
Viongozi wa utoaji huduma ya Maji ngazi ya Jamii CBWSOS Katika mkoa wa Katavi wamesema serikali kuja na Mpango wa Malipo ya Serikali kwa kutumia huduma za maji Vijijini unakwenda kuongeza Mapato ya Serikali kwakuwa malipo yote ya huduma za Maji zitakuwa zinalipwa kwa njia ya Mfumo kupitia simu za Mikononi.
Viongozi wa utoaji huduma ya Maji ngazi ya Jamii CBWSOS Katika mkoa wa Katavi wamesema serikali kuja na Mpango wa Malipo ya Serikali kwa kutumia huduma za maji Vijijini unakwenda kuongeza Mapato ya Serikali kwakuwa malipo yote ya huduma za Maji zitakuwa zinalipwa kwa njia ya Mfumo kupitia simu za Mikononi.
Wakizungunza katika mafunzo
elekezi ya namna ya kutumia mfumo wa malipo ya serikali kwa watumia huduma za
maji vijijini wamesema kuwa wakati mwingine imekuwa vigumu kuthibiti upotevu wa
malipo ya bili za Maji kwakuwa malipo mengi yalikuwa yanafanyika kwa njia ya
kulipa fedha Mkononi.
Viongozi wa jumuiya za watoa huduma ya Maji ngazi ya Jamii Mkoa wa Katavi wakiwa katika mafunzo ya Mfumo wa Malipo ya Serikali ambao umeanza kutumika kwa wateja wa Ruwasa |
Jackson Jozi Msimamizi wa Huduma ya watumia maji Kata ya Mpanda Ndogo Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi amesema kuwa mfumo huo utawarahishia kukusanya mapato kwakuwa utakuwa wazi kwa watumia maji kuliupa bili zao za Maji moja kwa moja kwenye Mfumo.
‘’faida ya mfumo huu ni mfumo
ambao upo wazi kiasi ambacho mteja amelipia ndio kiasi ambacho atatumia
tunaishukuru serikali kwa kuuleta Mfumo huu kwenye CBWSOS anasema Jozi’’
Kwa upande wake Frank Rafaeli
kiongozi wa jumuiya ya watumiamaji ameeleza kuwa mfumo wa GPG Utawasaidia
wateja wao kupata Bili zao za Maji kwa wakati pamoja na malipo yote ya serikali
kwenda moja kwa moja Serikalini.
Rafael ameishukuru serikali kwa
kuona umuhimu wa kuwaunganisha katika Malipo ya serikali hali ambayo itakwenda
kupunguza upotevu wa Mapato yaliyokuwa yanapotea kupitia huduma za Maji
Vijijini Ruwasa.
Kaimu Mratibu wa Ruwasa Mkoa wa Katavi,Ain Gick Shoo akielezea faida ya Mfumo wa malipo ya serikali kwa Taasisi ya Ruwasa namna utakavyoongeza Mapato kwa serikali |
‘’mfumo huu unafaida kubwa sana
mteja atalipia Maji kwa kutumia Control namba ambayo itasoma moja kwa moja GPG
hii itasaidia kwa kiwango kikubwa ukusanyaji wa Mapato ‘’amesema Busunzu
Pamoja na hayo amesema kuwa Mfumo
huo utasaidia kutambua wateja wao pamoja na Mchango wanao uchangia katika mfuko
wa Serikali wa Mapato kwakuwa mfumo huo utakuwa unatambua moja kwa moja mapato
yanayotokana na huduma za Maji vijijini kupitia Ruwasa.
Aamesema mafunzo hayo
yamefanyika katika Mikoa ya Rukwa, Shinyanga, Morogoro, Mwanza, Kilimanjaro,Katavi
ambapo watumiaji maji Vijijini watalipia
Huduma ya Maji kwa njia ya Mtandao.
Ain Gick Shoo Kaimu Mratibu wa Ruwasa Mkoa wa Katavi amesema jumuiya za watumiamaji zipatazo 26 zimepatiwa mafunzo hayo ya kulipia huduma za Maji kwa wateja wao kupitia mtandao ambao umeunganishwa na Mfumo wa Malipo ya Serikali GPG.