WANANCHI WAFURAHIA KUSOGEZEWA HUDUMA ZA AFYA

Shija Sabuni Mkazi wa Kijiji cha Kapanga akiwa katika zahanati ya Kijiji hicho alipomleta mtoto wake kwaajili ya kupatiwa huduma 

Na Mwandishi wetu-Katavi

Wananchi Kijiji cha Kapanga Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wameishukuru serikali kwa kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu kwa kujengewa zahanati kutokana na mapato ya ndani ya fedha za hewa ya ukaa.

Nyumba ya Mtumishi wa Afya katika kijiji cha Kapanga iliyojegwa kutokana na fedha za hewa ukaa.

Wananchi Kijiji cha Kapanga Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi wameishukuru serikali kwa kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu kwa kujengewa zahanati kutokana na mapato ya ndani ya fedha za hewa ya ukaa

Shija sabuni mkazi wa kijiji hicho ameeleza kuwa kabla ya kujengwa kwa zahanati hiyo ilikuwa ianawalazimu kusafiri umbali mrefu kwenda kupata huduma ya matibabu katika kijiji jirani cha Katuma.

’Tunashukuru sana zamani tulikuwa tunahangaika sana tunaenda Katuma sema kweli tunashukuru sana mimi nasema asanteni sana kwa kutuletea huduma hii hapa kijijini kwetu’’-Shija.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Shabani Juma akizungumnza na waandishi wa habari kuhusu namna fedha za hewa ukaa zinavyoisaidia Halmashauri kujenga miundombinu mbalimbali ya maendeleo kwa wananchi

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kijiji cha Kapanga Deus Hawazi amesema kuwa kujengwa kwa zahanati hiyo kunatokana na jitihada za utunzaji wa Mazingira kijijini hapo hali iliyopelekea kuanza kunufaika na Biashara ya Hewa ukaa.

‘’Tumenufaika sana na Uhifadhi wa mazingira baada ya kufanya matumizi bora ya aridhi tukatenga misitu ya Kijiji tumeweza kujipatia fedha nyingi sana kwaajili ya kuuza hewa ya ukaa iliyopelekea kujengwa kwa zahanati hii’’-Hawazi

Hawazi ameeleza kuwa katika kijiji hicho kuna baadhi ya wananachi wamekatiwa Bima ya Matibabu kupitia fedha za hewa ukaa ili kulahisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi Kijijini hapo.

Mwenyekiti huyo ameeleza kuwa ataendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kutunza mazingira ili waendelee kunufaika na fedha za hewa ukaa ambazo zimekuwazikiletwa kijijini hapo katika sekta ya Afya na Elimu.

Tinara Samweli Mganga mfawidhi wa zahanati ya Kapanga ameeleza kuwa tangu zahanati hiyo ianze kufanya kazi wamekuwa wakipokea wateja mbalimbali kwaajili ya kupatiwa Matibu kwenye zahanati hiyo.

‘’Tumeanza kutoa hapa tangu 27/11/2023 tulianza na wateja wachache lakini kwa sasa hivi tumeweza kuwahudumia zaidi ya wateja 1200 toka tuanze kutoa huduma hapa’’-Samweli

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Tanganyika Shabani Juma ameeleza kuwa kupitia Mapato ya ndani yanayotokana na fedha za hewa ya ukaa halmashauri hiyo imekuwa ikijenga Miundo mbinu ya Madarasa,Nyumba za watumishi na zahanati kwenye vijiji 8 vinavyonufaika na Biashara hiyo.

‘’Ukienda mwese Pale Lugonesi utakuta tumejenga Zahanati na Nyumba ya Mtumishi tumejenga pia ofisi ya serikali ya Kijiji hii yote ni miradi inayotekelezwa na fedha za mapato ya ndani kupitia biashara ya hewa ukaa’’-Shaban

Amebainisha kuwa katika kipindi cha Malipo ya awamu ya nane na Tisa halmashauri hiyo inatarajia kupokea kiasi cha Shilingi Bilioni 14 fedha zinazotokana na hewa ya ukaa ambazo zitakwenda kujenga miradi mbalimbali katika vijiji Nane vinavyonufaika na biashara ya hewa ya ukaa.

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages