WANANCHI WAKOSA MAKAZI BAADA YA ZIWA TANAGANYIKA KUJAA MAJI

Eneo la Mwambao wa ziwa Tanganyika Karema likionekana kujaa Maji kwenye eneo la Kingo hizo.

Na Walter Mguluchuma-Katavi

Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Karema Mwambao wa ziwa Tanganyika Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wamelazimika kukimbia kwenye makazi yao wanayoishi kwa kuhofia kusombwa na maji huku wengine kupewa makazi ya muda kwenye Shule ya Msingi baada ya ziwaTanganyika kujaa Maji na Kufika kwenye Makazi ya Watu.

Eneo la Makazi ya watu Kijiji cha Karema likionekana kuzingilwa na Maji

Baadhi ya Wakazi wa Kijiji cha Karema Mwambao wa ziwa Tanganyika Wilaya ya Tanganyika mkoa wa Katavi wamelazimika kukimbia kwenye makazi yao wanayoishi kwa kuhofia kusombwa na maji huku wengine kupewa makazi ya muda kwenye Shule ya Msingi baada ya ziwaTanganyika kujaa Maji na Kufika kwenye Makazi ya Watu.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Karema Sililo Mpondela amesema tukio hilo la ziwa Tanganyika kujaa Maji na kuzua taharuki kwa wananachi wa Kijiji hicho limetokea juzi kuanzia Saa tatu Asubuhi Hadi Saa Kumi Jioni.

Amesema siku hiyo ya tukio Mawimbi Makubwa yaliyotokana na kujaa maji kwenye ziwa hilo kulipelekea maji kufika hadi kwenye Makazi ya watu wanayoishi hali iliyopelekea baadhi ya Wananchi kukimbia Nyumba zao baada ya maji kujaa kwenye Makazi yao.

Mpondela amebainisha kuwa kufutia hali hiyo iliwalazimu baadhi ya wakazi wa Karema wanaoishi Jirani na ziwa hilo kukimbia kwenye Makazi yao baada ya Nyumba zao kuingiliwa na Maji na kuhamia kwenye nyumba za ndugu zao.

Huku familia Mbili zikihamishia Makazi yao kwenye shule ya Msingi baada ya kupewa makazi ya muda na uongozi wa Serikali ya Kijiji baada usalama wao kuwa hatarini kutokana na hali hiyo.

Ameeleza kuwa tukio hilo nilamara ya Tatu kutokea kwa kipindi cha Miaka Mitatu kwa kuwepo na ongezeko la Maji kwenye ziwa Tanganyika .

Kutokana na tukio hilo waathirika wa tukio hilo wameobwa na uongozi wa serikali ya kijiji kutorudi kwenye makazi yao mpaka pale hali itakapo tengemaa huku wakihofia wananchi hao kupatwa na magojwa ya Mlipuko. 

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages