WANANCHI 35000 KUNUFAIKA NA HUDUMA YA MAJI

 

Mkuu wa Wilaya ya Tangayika Onesmo Buswelu akimtishwa ndoo ya Maji Mwananchi wa kijiji cha Mpembe

Na walter Mguluchuma-Tanganyika

Wakala  wa  Maji  na Usafi wa  Mazingira   Vijijini (RUWASA)   Wilaya ya  Tanganyika inatarajia  kutekeleza  miradi   minne  inatakayo wanufaisha  jumla ya  Wananchi 35,468 katika Vijiji  nine  ambavyo  havina  miundombinu ya  maji   itakayogharimu kiasi cha  shilingi BILIONI 5.3  itakayoongeza  upatikanaji wa   maji  katika  Wilaya ya Tanganyika  kutoka  asilimia  78 hadi kufikia  asilimia  86.

Hayo ameyabainisha  Meneja wa  RUWASA   Mhandisi   Tiuway   Ninga  wakati  uzinduzi wa   huduma ya  maji   katika    Kijiji  cha  Mpembe   Kata ya Katuma  ambao  utawanufaisha zaidi ya watu 4000 uliogharimu kiasi cha  tshs  210,422,433.

Ninga Amesema  RUWASA  Wilaya ya  Tanganyika    katika  mwaka wa fedha 2024/2025 wanatarajia kutekeleza   miradi    minne   ambayoitawanufaisha  watu 35, 468 itakayotekelezwa   kwenye  vijiji vine  na kugharimu kiasi cha tshs  5,385,714,753.27.

amesema  hali  ya  upatikaji wa  maji kwa sasa katika  Wilaya ya  Tanganyika  ni  asilimia  78 hivyo  miradi hiyo  itaongeza  hali ya  upatikanaji wa  maji  safi na  salama  kufikia  asilimia  86 hadi kufikia hapo mwakani .

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo Buswelu akizindua huduma ya     Maji Kijiji cha Mpembe Kata ya Katuma Halmashauri ya wilaya ya Tanganyika 

Mhandisi  Ninga  ameeleza kuwa  mradi  wa  Maji uliozinduliwa kutowa huduma ya maji  utakao wanufaisha watanchi   4000 wa  Kijiji  cha  Mpembe  amesema mradi  huo umewezesha  upatikanaji wa  huduma  ya  maji safi na  salama  kwa wananchi wa  Kijiji cha  Mpembeb  na kuweza kupata manufaa  mbalimbali .

Ameyataja  baadhi ya  manufaa hayo kuwa ni  kumewapunguzia   umbali  mrefu  na muda   wa kutafuta  maji hivyo  kupata  muda  kufanya  shughuli nyingine  za  kiuchumi kupata maji safi na salama .

Manufaa mengine ya mradi huo  ni  kuondokana  na  maradhi  yatokanayo  na  matumizi  ya  maji  yasiyokuwa  safi na salama  na uimarishaji  wa  mahudhurio  yatokanayo na wanafunzi  mashuleni  hasa  katika  shule ya  Msingi  Mpembe .

Mradi huo wa Maji Mpembe  umegharimu   kiasi cha tshs   210,422,433   umetekelezwa  na  Kampuni  ya  Mkandarasi   Kabansora  Construction  Company  Limeted ya  Dar es salamu

Meneja wa RUWASA Wilaya yaTanganyika Mhandisi Tiuway Ninga akitoa Taarifa ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa mgeni rasimi Mkuu wa wilaya ya Tanganyika 

Miundo mbinu  ambayo imejengwa    hadi sasa  ni  ujenzi wa tanki   lenye uwezo wa   kuhifadhi  lita za ujazo  135,000 pamoja  uzio wa kuzunguka  tanki ,ujenzi  wa vituo vitano  vya kuchotea maji   vyenye  jumla ya  vichocheo   10, ununuzi wa pampu  na ufungaji wa nishati ya umeme wa jua .

Kwaupande wao wananchi wakijiji hicho wanazungumzia upatikanaji wa huduma ya maji Vitus  Joseph ni  mkazi wa Kijiji cha Mpembe amesema  upatikaji wa  huduma ya maji kwenye  Kijiji  hicho  utasaidia kumtuoa  mama   ndoo kichwani  na kutaondoa changamoto ya ndoa. 

Roza Mbalamwezi amesema tatizo la kutokuwa na maji  kwenye eneo hilo wanaloishi  likuwa  ni kero kwenye familia nyingi kutokana na akina mama kutumia muda mrefu kwenda kutafuta maji umbali mrefu  hali iliyokuwa ikiwaletea akina mama kero kubwa kutoka kwa waume zao walikuwa wake zao kuchelewa kurudi nyumbani .

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Onesmo  Busweru  amesema  upatikanaji  wa vyanzo vingi vya  maji  katika  Wilaya ya Tanganyika umetokana na kazi kubwa inayofanywa katika Wilaya hiyo ya kuhakikisha  mazingira yanakuwa salama muda wote .

Amesisitiza kuwa  watahakikisha wanaendelea kufanya dolia za  mara kwa  mara  za kulinda mistu  na  mtu yeyete ambae  atakae kamatwa akifanya uharibifu kwenye mistu na kwenye vyanzo vya maji hawatakuwa na huruma nae watamchukulia hatua kali za kisheria .

Amesema wananchi wa  Kijiji hicho hawakuwa na  maji kwa  muda  mrefu lakini  serikali ya awamu ya sita kwa  kuliona hilo ndio maana imewapelekea  huduma hiyo ya maji safi na salama kwenye kijiji hicho .

Search This Blog

CHAGUA HABARI

Pages